bayyinaat

Published time: 20 ,October ,2017      08:45:11
Baada ya kufahamu kwamba dini ya Kiislamu siku zote imekuwa ni yenye kuweka mifumo sahihi kwa wana familia ili kuweza kufikia malengo makubwa, sasa ni wakati wa kuweza kufahamu kwamba.........
News ID: 118


Baada ya kufahamu kwamba dini ya Kiislamu siku zote imekuwa ni yenye kuweka mifumo sahihi kwa wana familia ili kuweza kufikia malengo makubwa, sasa ni wakati wa kuweza kufahamu kwamba kuna watu ambao kwa kutumia akili zao za kawaida wamejaribu kuja na mifumo yao ya kifamilia wakiwa na imani kwamba ni mifumo sahihi hali ya kuwa mambo ni kinyume kabisa, bali tunakuta ni mifumo ambayo inaharibu na kubomoa kabisa familia za wanadamu.

Ifuatayo ni baadhi ya mifumo hiyo pamoja na athari zake katika familia n akwa jamii kwa ujumla.

1.   Mfumo wa Marcus

Huu ni mfumo ambao tunaweza kuuita janga katika familia na jamii nzima za wanadamu, kwa maana msingi mkubwa wa mfumo huu ni kuhakikisha kwamba mtoto tangia akiwa mdogo basi analelewa katika maisha ya kwamba anatakiwa ajitambue kwamba yeye ni mkazi tu na wala hana mahusiano na familia yeyote ile.

Hivyo mtoto baada ya kuzaliwa hawi ni mwanafamilia wa familia fulani, bali huwa ni mkazi tu wa jamii ile.

Maulama wa elimu za jamii wanaukosoa mfumo huu kwa kusema ".....Ikiwa mambo yatafikia katika hali hii, basi jamii nzima itaanguka, na pia hakutakuwa na familia thabiti, kwa maana moja ya nguzo muhimu katika familia inakuwa imeanguka....”.

                                                                                     Rejea kitabu Al Usratul wal Mujtamaa uk 14

Ndio, hakuna familia wala jamii ambayo itaweza kusimama bila ya nguzo, kwa maana mtoto kama mtoto ni nguzo muhimu katika kujenga familia na jamii kwa ujumla kama tulivyotanguliza, sasa endapo mtoto atakuwa ni fikra ya kwamba yeye si wa familia fulani bila shaka atakuwa na fikra ya kwamba yeye si wa jamii fulani pia, hivyo mwisho wa siku hakutakuwa na familia wala jamii iliyo thabiti.

2.   Mfumo wa Masson "Masonism”

Huu pia ni mfumo ambao unalenga moja kwa moja katika kumtenganisha mwanadamu na familia yake. Haya si maneno yangu mimi , bali tunayakuta endapo tutarejea katika hotuba ya mwenyewe Mason ambayo aliitoa mnamo mwaka 1921 alipokuwa akiwapa watu njia za kuweza kutenganisha baina ya familia na nguzo zake.

Anasema ".......Ili muwe na uwezo wa kutenganisha baina ya familia ni lazia kwanza muweze kuondoa maadili na misingi yake kwa familia hizo kwa kutumia mambo ambayo yamekatazwa kwao, na hii ni kutokana na kwamba nafsi za wanadamu siku zote huwa zinapenda kuelemea yale ambayo zimekatazwa kwayo,  kama vile kukata mahusiano n akukaribia kila lililo chafu. Kama ambavyo pia nafsi hizo hupendelea zaidi mambo ya kila mmoja kuwa kivyake kuliko mambo ya kushikamana katika familia au jamii moja, au kukaa na kupiga porojo katika vijiwe kuliko kusimamia mambo yanayohusu familia zao. Sasa watu kama hawa unaweza kuwahadaa kwa kuwaahidi nafasi na nyadhifa kubwa na hata vipato vikubwa kutoka kwetu.........”

                                                                    Rejea Utangulizi wa kitabu cha Istratijiyatul Usra uk 11

Nadhani umejionea mwenyewe jinsi gani watu walivyo na nia thabiti katika kuharibu familia n ajamii kwa ujumla, tena hata kwa kutumia gharama kubwa kabisa katika hilo. Cha msingi ni kwamba inatakiwa tuelewe ya kuwa kila mfumo ambao unakuwa unapingana na mfumo sahihi wa familia na jamii, au kila mfumo ambao utakuwa hauelewi kwa usahihi misingi na malengo ya familia basi inatakiwa tuutupilie mbali, kwa maana bila shaka utakuwa ni mfumo wenye kutuangushia katika majanga na machafuko ya kifamilia na kijamii kwa ujumla.

 

maoni Viewers
Name:
Email:
* Opinion: