bayyinaat

Published time: 20 ,October ,2017      08:57:27
Ni jukumu la kila mpenda maendeleo ya familia n ajamii yake kwa ujumla kuweza kutoa juhudi zake katika kuhakikisha kwamba familia yake na jamii yake kwa ujumla inatilia umuhimu swala zima la........
News ID: 119


Ni jukumu la kila mpenda maendeleo ya familia n ajamii yake kwa ujumla kuweza kutoa juhudi zake katika kuhakikisha kwamba familia yake na jamii yake kwa ujumla inatilia umuhimu swala zima la hisia za wahusika wake. Kwanini nasema hivi?, na kwa sababu hisia za mwanadamu hasa katika swala la kupenda kuwa na mahusiano ni kali sana kuliko tunavyofikiria, n anaweza kusema kwamba ni swala ambalo linawasukuma wengi sana kufanya mambo yaliyo mengi. Mfano leo hii utakuta kuna asilimia kubwa ya watu ambao wanafanya juu chini waweze kupata kipato, nafasi kubwa, nyadhifa n a hata majina, lakini lengo kubwa ni ili tu waweze kufikia katika kutimiza hisia zao kwa wale ambao wanaamini ndio sahihi kwao. Pia hata ukija kwa ambao tayari wapo katika familia zao bado utakuta kwamba jambo ambalo linapelekea kuendelea kubakia kwa upendo, amani, masikilizano ndani ya familia hizo ni swala zaima la hisia, n a laiti kama kusingalikuwa na hisia hizo basi kusingalikuwa na upendo ambao ulikuwepo wakati hisia hizo zilikuwepo baina yao. Najua unaweza ukawa bado hujakubaliana nami katika hili, ila nitakupa mfano wa mwisho wa kuweza kukufanya ukubaliane nami, angalia leo hii watu ambao tunawaita ni "waliofiwa na hisia zao”, yaani wale watu ambao hawana hisia kabisa za kuwa karibu na wengine, jinsi gani ambavyo wanateseka na kutaabika katika maisha yao, wenyewe ukiwauliza kunako jambo hili watakujibu kwamba wapo salama na wanafurahia maisha yao, lakini si kweli, ni kwamba wanakuwa na matatizo makubwa sana kijamii. Na kama isingalikuwa ni tatizo basi kusingalikuwa na mahospitali makubwa ulimwenguni ambayo yanahusika na kutibu tatizo hili. Ni kwamba wamekaa na kuchunguza watu wa namna hii na kukuta kwamba kuna baadhi ya matatizo hayatoki isipokuwa kwa watu hawa tu.

Hivyo basi ni jukumu la kila mwana familia kuweza kuhakikisha kwamba nguzo za familia yake zinajijenga katika mahusiano sahihi na ambayo ni yenye kuruhusiwa na misingi sahihi ya familia na dini kwa ujumla, kwa maana huwezi kuisemea nafsi ya wanafamilia wako kwa  kusema kwamba mtoto wangu au mwenza wangu  hana fikra wala mawazo ya kufuata hisia zake, kumbuka kwamba hisia za wanadamu katika swala la mahusiano ni kali mno. Na endapo mwanafamilia hatokuwa makini katika jambo hili basi atajikuta mwisho wa siku anajuta kwa kukuta kwamba moja ya nguzo za familia yake imefuata ukali wa hisia zake na kuangukia katika mahusiano ambayo si sahihi kwake.

Mahusiano ambayo si sahihi

Kama tulivyotanguliza ni kwamba kila mwanafamilia anatakiwa kuwa makini katika kuhakikisha kwamba nguzo za familia yake zinashikamana na mahusiano ambayo ni sahihi. Hapa tulikuwa tunajaribu kulenga kwamba kuna mahusiano ambayo si sahihi katika jamii, na mwisho wa mahusiano haya ambayo si sahihi ni kuharibu na kuvunja misingi ya familia n a jamii kwa ujumla kutokana na athari zake mbaya.

Tutajaribu kuelezea baadhi ya mahusiano hayo ambayo si sahihi pamoja na athari zake zinazoambatana nayo.

kuwa nasi katika wakati ujao......

maoni Viewers
Name:
Email:
* Opinion: