Kama
tulivyotanguliza ni kwamba kila mwanafamilia anatakiwa kuwa makini katika
kuhakikisha kwamba nguzo za familia yake zinashikamana na mahusiano ambayo ni
sahihi. Hapa tulikuwa tunajaribu kulenga kwamba kuna mahusiano ambayo si sahihi
katika jamii, na mwisho wa mahusiano haya ambayo si sahihi ni kuharibu na
kuvunja misingi ya familia n a jamii kwa ujumla kutokana na athari zake mbaya.
Tutajaribu
kuelezea baadhi ya mahusiano hayo ambayo si sahihi pamoja na athari zake
zinazoambatana nayo.
1.
Zinaa
Moja kati ya mambo ambayo huhesabika ni katika mahusiano
ambayo si sahihi ni swala zima la uzinzi au zinaa, kwa lugha ya sasa wanaita
(michepuko) kwa maana ya mahusiano yasiyo rasmi.
Kwanza nishukuru kuona
kwamba wenyewe wanakubali kwamba kitendo hiki ni kuchepuka na kutoka katika
njia kuu, kisha ndipo niweke wazi kwanini wenyewe wanasema ni kuchepuka. Bila
shaka wanajua kwamba kitendo hiki ni kufanyia hiyana familia yako, jambo ambalo
si jema kiakili hata kidini pia, pia
kuna athari nyingine ambazo zinakuja kama vile kukosa heshima ya watoto wake,
kupungua mapenzi yake kwa familia yake n a mengineyo. Lakini cha kushangaza ni
kwamba jambo hili la zinaa ndilo jambo ambalo limeenea sana katika vizazi vya
zama hizi kama ambavyo Muhammad bin Farid Wujdiy anasema "....Jambo la
kusikitisha mno ni kwamba swala la zinaa ndilo ambalo limechukua sura mno n
akuenea katika karne hii pamoja na mambo mengine ambayo hayaendani na mfumo
sahihi wa maisha ya wanadamu....”
Ndio, leo hii vijana ambao
tayari wamefikia umri wa kuoa hawataki kabisa kusikia jambo hilo, wakiwa na
hoja ya kwamba wakijiingiza katika ndoa basi maisha yatawaendesha sana na
watatakiwa wafanye kazi mno, au wakati mwingine hutoa hoja ya kwamba kama
wakitaka kuoa hali ya kuwa hawana maisha mazuri na kipato kizuri cha pesa basi
watashindwa kuoa katika familia au nyumba za wenye uwezo wao kimaisha. Hivyo hutumia
muda mwingi sana katika kutafuta vipato, majina, au maisha mazuri ili tu waweze
kuoa hao ambao wanawafikiria. Lakini wanasahau kwamba wakati ambao yeye
anajishughulisha na kutafuta hayo maisha mazuri, si kwamba zile hisia kali
zinampa nafasi pia, bali zinaendelea kumshawishi na kumsukuma kuelekea upande
uutakao, hivyo kujikuta huku akisubiri mke wa ndoto zake hapa kati anakuwa
amefanya mambo mengi sana ambayo si sahihi kwake (kama ilivyo kwa vijana wengi
sana wa sasa).
Cha muhimu ni kwamba kila
familia na jamii kwa ujumla kuweza kuweka mifumo sahihi ya kuweza kuepukana na
janga hili kubwa ambalo hakuna jamii ambayo itashikamana nalo ila ni kwamba Mwenyezi Mungu ataiadhibu jamii
ile kwa aina mbalimbali za adhabu. Hii ni ukiachilia bali adhabu ambazo Uislamu
umeziweka kwa kila mwenye kufanya kitendo hicho na kwa masharti yake ambayo
yameelezewa kwa kirefu katika surat Al Nur aya ya 2 pale Mwenyezi Mungu
aliposema:
الزَّانِيَةُ وَالزَّانِي فَاجْلِدُوا كُلَّ وَاحِدٍ
مِنْهُمَا مِائَةَ جَلْدَةٍ ۖ وَلَا تَأْخُذْكُمْ بِهِمَا رَأْفَةٌ فِي دِينِ
اللَّهِ إِنْ كُنْتُمْ تُؤْمِنُونَ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ ۖ وَلْيَشْهَدْ
عَذَابَهُمَا طَائِفَةٌ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ
"....Mzinifu mwanamke na
mzinifu mwanamume, mtandikeni kila mmoja katika wao bakora mia. Wala
isikushikeni huruma kwa ajili yao katika hukumu ya Mwenyezi Mungu, ikiwa nyinyi
mnamuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho. Na lishuhudie adhabu yao kundi la
Waumini...”
Pamoja n akwamba kuna
ambao wanajiona wao ni wajuaji wakubwa wa haki na wenye huruma kubwa sana kwa
wanadamu, ambao wanakuja na kusema kwamba hukumu hii ni yenye kuonea na
haiendani kabisa na huruma kwa wanadamu. Ati!!, hivi kuna mwenye huruma kwa
viumbe zaidi ya aliyeviumba?, lazima itambulike kwamba hukumu hii ni yenye
kulenga kutengeneza familia na jamii iliyo bora zaidi, je kuna huruma zaidi ya
hii?, hivyo basi ikiwa kuna jambo lolote ambalo linataka kuja kuharibu yale
yaliyo bora kwa wanadamu ni lazia likemewe na lichukuliwe hatua kali.
2.
Kuingiliana kinyume na maumbile
Moja kati ya mifumo ambayo
inakuja kupiga vita n a kutokomeza kabisa mfumo sahihi wa maisha ya kifamilia
na kijamii kwa ujumla ni mfumo wa wanadamu kuchagua maisha ya kuingilia na
kinyume na maumbile wao kwa wao au kwa ibara nyingine ni mapenzi ya jinsia moja.
Kwa maana baada ya jambo
hili basi hakutakuwa tena na malengo ya kufikiria kujenga familia au jamii kwa
ujumla. N a hapa naongelea kwa ujumla kabisa, iwe anayefanya jambo hili ni mtu
ambaye tayari ana familia yake, au awe hana familia. Kwa maana kama atakuwa na
familia yake kisha akashiriki jambo hili huko nje bila shaka zile athari za
kutokuwa na mapenzi na familia yake na nyinginezo bado zitaambatana naye, na
kama atakuwa hana familia basi ndio kabisa, maana hata hiyo fikra ya kuwa na
familia na jamii hatokuwa nayo.
Lakini kwa zama hizi swala
la mapenzi ya jinsia moja ni swala ambalo limeshika kasi sana, tunaambiwa
katika baadhi ya nchi za Ulaya, kuna wanasheria ambao husimama kidete katika
kutetea jambo hili, hali ambayo imepelekea kuona baadhi ya watu wakiacha familia
zao na kutafuta vijana ambao wanaoana nao n a kuendeleza mahusiano ya jinsia
moja. Sasa hiki kitendo cha mtu kutelekeza familia yake ni moja tu ya athari
ambao zinatokana na jambo hili baya. Bado kuna adhabu za Mwenyezi Mungu juu ya
mshiriki wa kitendo hiki kama vile:
a.
Kuuwawa kwa upanga
b.
Kuchomwa moto
c.
Kuangushiwa ukuta
d.
Kutupwa kutoka juu ya jengo refu
Na ambaye anafanyiwa
kitendo hiki kama atakuwa ni mwenye kubalehe na ana akili timamu basi ni lazima
auwawe, n akama atakuwa hajabalehe basi kuna hukumu zake maalumu ambazo unaweza
kurejea vitabu vya hukumu.
Muhimu ni kwamba jambo
hili ni katika ambo ambayo yanaharibu kabisa misingi na malengo ya familia na
jamii kwa ujumla, na linatakiwa likemewe kwa nguvu zote.
itaendelea......