bayyinaat

Published time: 05 ,March ,2017      23:09:40
Tunahitaji mtu asiyefanya dhambi na asiyekosea, mtu ambaye kwamba hata tukichungua kiasi gani utu wake, hatuwezi kuona hata dalili ya hitilafu katika mpango wake, ambao wingi wa tabia zake za maisha hufanya picha tukufu kwa ajili ya macho yetu kutazama na roho zetu kujipatia mwongozo mwema..........
News ID: 34

Kila siku binadamu anatafuta mwongozo. Kutafuta huku humfanya binadamu huyu aonane na binadamu wengine wengi, hivyo kwamba tunaweza kukulinganisha huku kujaribu kwake zaidi au kidogo na kuhangaika kwa mtu mwenye kiu katika jangwa lisilo na maji, ambaye anadanganywa na mazigazi, (sarabi) mia moja na moja. 

Tunahitaji mtu asiyefanya dhambi na asiyekosea, mtu ambaye kwamba hata tukichungua kiasi gani utu wake, hatuwezi kuona hata dalili ya hitilafu katika mpango wake, ambao wingi wa tabia zake za maisha hufanya picha tukufu kwa ajili ya macho yetu kutazama na roho zetu kujipatia mwongozo mwema. 

Mtu huyo ni lazima awe katika bali ambayo kila binadamu duniani kote aweze kupata mfano wa kufuata. Tunapolinganisha na kuamua ni yupi kati ya watu mashuhuri duniani, tunaona kwamba uwezo wa uongozi wao unafikia kiwango fulani tu cha kazi zao na nguvu zao za uongozi. Tunaweza tukamtaja Vikramaditya kama mfano wa mfalme mwadilifu lakini mfano wake ni kwa wafalme tu; au tunaweza kumtaja Asoka kama bingwa wa amani walakini anashindwa kutupa matumaini tunapojaribu kumfikiria kama kiongozi mashuhuri wa nchi; na wote hawa wawili waliotajwa hapo juu wanashindwa kutupa mfano kwa raia. Au tunaweza kumtaja Mtakatifu Petro kama roho chamungu lakini atawezaje kutuongoza kama tukikabiliwa na machafuko ya kitaifa? Tunaweza pia kuwataja wapiganaji na watekaji mashuhuri lakini majinayao hayatakuwa na maana kwetu tukihitaji mfano wa mtu mwenye uvumilivu na uwezo wa kuvumilia taabu na mateso. 

Kwa kifupi, tunaweza kupata watu walio nyota zitumulikazo kwa nuru ya sifa za utu moja au zaidi, lakini historia itashindwa kutuonyesha jina linaloweza kuwaongoza, watu wote waishio katika mazingira ya namna mbalimbali isipokuwa Hadhrat Ali bin Abi Talib (Amani ya Mwenyezi Mungu na iwe juu yake) tu.

Hapa tunatoa kwa ufupi tu maisha ya ajabu ya mtu huyu wa ajabu mwenye uwezo wa kufahamu mambo mengi ambaye walimwengu wanapasika kumjua na kumpendelea.

Nasaba yake

Hadhrat Ali (a.s.) alikuwa mwana wa Bwana Abu Talib mwana wa Abdul Muttalib wa ukoo wa Hashim ambao ulikuwa wa kabila la Quraish mtu aliyekuwa na nguvu sana na aliyeheshimiwa, aliyetokana na kizazi cha Nabii Ibrahimu (a.s.). Mama yake Hadhrat Ali (a.s.) ni Bibi Fatimah binti yake Bwana Asad, mwanamke aliyeheshimiwa na aliyekuwa wa ukoo wa Hashim. Hivyo Mtukufu Mtume (s.a.w.) na Hadhrat Ali (a.s.) ukoo mmoja. 

 

 

ABDUL MUTTALIB

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Abdullah

 

Abu Talib

 

 

 

 

 

Mtukufu Mtume Muhammad [s]

 

Ali

 

 
 

Zaidi ya hayo Bwana Abu Talib ndiye aliyemlea Mtukufu Mtume (s.a.w.) tangu baba yake alipofariki dunia kabla hata ya kuzaliwa kwake Hadhrat Ali (a.s.). 

Kuzaliwa kwake

Mtume (s.a.w.) alikuwa na umri wa miaka thelathini alipozaliwa Hadhrat Ali (a.s.) ndani ya Kaaba mnamo tarehe 13 mwezi wa Rajabu mwaka wa 30 Aamul-Fiil (sawa na mwaka 600 Miladiya). Wazazi wake walifurahi sana kuona kuwa mwana wao alikuwa anapendwa sana na mwana wa ndugu yao (yaani Mtukufu Mtume s.a.w.) ambaye alikwishagundua kutokana na uso wa mtoto huyo (Ali a.s.) ushupavu na nguvu vitu ambavyo vitamfanya kuwa msaidizi mkubwa utakapokuja mwito kutoka Mwenyezi Mungu.

Kulelewa kwake. 

Kwa sababu ya matuchumi ya Bwana Abu Talib, Hadhrat Ali (a.s.) alilelewa na Mtukufu Mtume (s.a.w.) ambaye alimpenda na kumtunza vizuri sana kijana huyu aliye binamu yake. Akamwongoza katika fikara zile zile zilizouongoza moyo wake. 

Waujumbe: 

Ilikuwa ni matokeo ya malezi (mema kutoka (wa Mtume s.a.w.) kwamba katika umri wa miaka kumi Hadhrat Ali (a.s.) alisikia Mtukufu Mtume (s.a.w.) akitangaza kuwa amechaguliwa kulichukua Neno Ia Mwenyezi Mungu na kuwataka watu wake waamini na kumuunga mkono. Ilikuwa ni mvulana huyu mwenye umri wa miaka kumi, aliyekuwa na ushupavu wa kusimama tayari kutii na kufuata (utume wa Mtume s.a.w.) na hivyo basi akawa shahidi wake wa kwanza, msaidizi wake na mrithi wake. Sauti ya Hadhrat Ali  (a.s.) ilikuwa (ndio) ile sauti iliyopazwa ili kumpa Mtukufu Mtume (s.a.w.) msaada wake familia yake, kabila lake, jamii yake, jiji lake, na hata watu wote Uarabuni kote walipompinga vikali. 

Nyakati za shida

Mara tu baada ya Mtukufu Mtume (s.a.w.) kutangazia Ujumbe wake upinzani ulianza pande zote. Watu ambao mpaka jana yake, kabla ya kuutangaza Ujumbe huo walimheshimu kwa sababu ya ukweli na uaminifu wake, sasa walianza kumwita mnafiki, kichaa, mchawi na kwa nini wasimuite hivyo? Walianza kuweka miiba katika njia yake, walimpiga mawe na hata kumtupia taka taka kichwani kwake. Katika dhidi yote hii kijana mwenye umri wa miaka kumi ndiye sahaba peke yake aliyelichukua Neno la Mwenyezi Mungu. Hadhrat Ali (a.s.) katu hakukata tamaa na kila mara alikuwa karibu zaidi na Mtume (s.a.w.). Hatimaye, wakati ulifika ambapo watu wa Maka waliamua kumgomea Mtume (s.a.w.) na familia yake. Bwana Abu Talib alimchukua Mtume (s.a.w.) na watu wake na kuwapeleka kwenye bonde (Iiitwalo (Shaab Abi Talib) lililokuwa jirani na jiji la Maka na kuishi huko kwa muda wa miaka mitatu wakiwa wametengwa kahisa na watu wengine. Waliishi katika hatari ya kila mara ya kushambuliwa na maadui wao wakati wa usiku. Hivyo, ili kumkinga Mtume (s.a.w.) na dhara lo lote lile liwezalo kutokea, Bwana Abu Talib alikuwa akichukua hadhari ya kumhamisha Mtume (s.a.w) kutoka kitanda kimoja hadi kingine kila usiku na kitandani pake Mtume (s.a.w.) alikuwa akimlaza mmoja wa wanawe. Kutokana na hayo, Hadhrat Ali (a.s.) alijifunza jambo ambalo alikuwa akilikariri kila mara katika maisha yake.

Hijrah 

Baada ya kifo cha ami yake mpenzi Bwana Abu Talib, Mtume (s.a.w.), ilimbidi kukutana na dhiki na matatizo makubwa na maadui zake wakawa wakatili zaidi. Siku moja maadui wa Mtume (s.a.w.) waliamuwa kuizunguka nyumba yake na kumuua akiwa usingizini. Mtume (s.a.w.) alipopata hatari hizi alimwita Hadhrat Ali (a.s.) na akamwambia aIale kitandani pake badala yake yeye Mtume (s.a.w.) aondoke kimya kimya kwenda Madina. Hadhrat Ali (a.s.) alimuuliza Mtume (s.a.w.), "Je, Mpango huu utayaponyesha maisha yako, ewe Mtume wa Mungu? Alipopata jibu la kumthibitishia kuwa Mtume (s.a.w.) atasalimika, Hadhrat Ali (a.s.) alilala usingizi mzito (wa furaha kitandani pa Mtume (s.a.w.). 

Usika wote ule Machifu wa Makuraishi waliokuwa na hamu ya kumwaga damu, walingojea mpaka kuche na waingie ndani na kumuua Muhammad (s.a.w.) Lakini asubuhi yake wale maadui waliona kuwa yule waliyekuwa wakimngojea alikwishaondoka na badala yake walimkuta Hadhat Ali ambaye walimdhania kuwa ni yeye Mtume (s.a.w.). Maadui hao walimwuliza Hadhrat Ali (a.s.) alikokwenda Mtume (s.a.w.). Hadhrat Ali (a.s.) aliwauliza maadui hao swali badala ya kuwapa jibu la swali lao akiwauliza kama walimuweka kuwa mchunga wa Muhammad. Hivyo maadui hao walirudi makwao huku wakiwa wamejaa hasira na wasi wasi. Mtume (s.a.w.) alifaulu kwenda mwendo mrefu bila ya matatizo yo yote. Hadhrat Ali (a.s.) alibaki mjini Maka kwa muda wa siku tatu zaidi na aliutumia muda huo kuwarudishia wenyewe vitu vilivyowekwa amana kwa Mtume (s.a.w.). Baada ya hapo Hadhrat Ali (a.s.) aliondoka kwenda Madina kwa miguu akiongoza msafara wa ngamia waliowabeba wanawake wa nyumba yake. Alipofika Madina miguu yake ilikuwa inatoka damu na nyayo zake zilikuwa zikitoka malengelenge. Hii inaonyesha imani Mtume (s.a.w.) aliyokuwa nayo juu ya Hadhrat Ali (a.s.) na nguvu na ujasiri vita ambavyo Hadhrat Ali (a.s.) alivithibitishia imani yake hiyo.  

Ndoa yake: 

Mtume (s.a.w.) alipofika Madina, kitu cha kwanza kumuoza binti yake Bibi Fatimah (a.s.) kwa Hadhrat Ali (a.s.). Mtume (s.a.w.) alimpenda sana binti yake na kila mahali alipomjia, Mtume (s.a.w.) alisimama ili kuonyesha heshima yake kwake. Kwa hiyo, kila mmoja alitazamia kumuoa Bibi Fatimah (a.s.) na wengine waliwahi hata kupeleka posa zao kutaka kumuoa binti wake Mtume (s.a.w.). Lakini Mtume (s.a.w.) alimwambia kwamba binti yake hawezi kuolewa bila ya ruhusa ya Mwenyezi Mungu. Ilikuwa katika mwaka wa kwanza wa Hijira Hadhrat Ali (a.s.) alipochaguliwa kutunukiwa heshima hii ya kumuoa binti yake Mtume (s.a.w.) na harusi ilifanyika katika njia rahisi sana. Binti yake Mtume (s.a.w.) hakufungashiwa hata vyombo vya nyumbani na baba yake, bali vile vyombo vya nyumbani alivyovipata vilinunuliwa kutokana tu na fedha aliyoitoa Hadhrat Ali (a.s.) kwa ajili ya "Mahari". Vyombo hivyo ni pamoja na vyungu vya udongo wa mfinyanzi vichache, mito michache ya majani ya mtende, kitanda cha ngozi, gurudumu Ia kusokotea nyuzi za sufi, kijaa na kiriba. Na Hadhrat Ali (a.s.) aliuza deraja yake ili kupata fedha ya kulipia mahari. Kwa hiyo, ulikuwa mfano kwa Waislamu wote ili kutumia akili katika matumizi yao na kuepuka kutumia pesa zao holela wakati wa sherehe za harusi.  

Itaendelea...

maoni Viewers
Name:
Email:
* Opinion: