bayyinaat

Published time: 05 ,March ,2017      23:37:29
Ibun Sina (Avicena) alizaliwa mwaka 370 A.H Sehemu ya Balakh ambayo ilikuwa ndani ya taifa la Iran ya zamani, ambapo hivi sasa ni ndani ya nchi ya Afghanistani, baba yake alikuwa ni katika mwana siasa na ni miongoni mwa............
News ID: 35

Maisha ya  Ibn sina (Avicnena)

Makala iliopita tulieleza kwa ufupi Historia ya Tiba katika Uislamu, na kuashiria baadhi ya madaktari waliopatika katika ulimwengu wa Kiislamu, ambapo miungoni mwao alikuwa ni daktari mahiri, mashuhuri Ibun Siina (Aviccena).

 Ama katika makala hii nitazungumzia maisha yake kwa ufipi na kugusia baadhi ya nukta muhimu za Elimu ya Tiba katika Qur'an na mtazamo wake kunako masuala ya Tiba na taaluma mbalimbali za kisayansi, hivyo basi nakuomba ndugu msomaji kuwa pamoja nami  katika kuangalia misingi ya Kiislamu kunako Elimu za Tajiruba na sayansi.

Ibun Sina (Avicena) alizaliwa mwaka 370 A.H Sehemu ya Balakh ambayo ilikuwa ndani ya taifa la Iran ya zamani, ambapo hivi sasa ni ndani ya nchi ya Afghanistani, baba yake alikuwa ni katika mwana siasa na ni miungoni mwa wanazuoni maarufu wa zama zake, Ibun Sina (Avicena) alilelewa katika mazingira ya kiimani sambamba na mashiko halisi ya dini ya kiisilamu, ambapo katika miaka kumi ya awali alijifunza Qur’an na elimu za kilugha, pia alijifunza  Elimu za kiakili na hesabu kwa bwana Mahmudi  Masaha na kusoma Elimu ya Mantiki  kwa bwana Natly, pia kujifunza alimu za Sheria na Kifikihi kwa sheikh Ismail Zahid katika sehemu hiyo.

Imeelezwa kuwa Avicenna alisoma kitabu cha Arustrit mara arubaini, pia alikuwa anachunga sana masuala ya Imani, Dini na Sheria zake, naye alikuwa mtu wa ibada sana na mwenye jitihada katika kutafsiri  Qur’an na kuihifadhi na kujifunza Elimu ya Hadithi. Alianza kujifunza Utabibu na Udaktari akiwa na umri wa miaka 16 naye alikuwa akisema: katika muda mchache nilipokuwa ni kujifunza Elimu ya Tiba nilipata umahiri na uwezo mkubwa wa Elimu hiyo, na nikapata umaarufu mkubwa na kufahamika sana katika kutibu wagonjwa.

Avicenna aliendelea na harakati zake hizo mpaka mnamo mwaka 428 A.H akafariki na kuitika wito wa mola wake. Ama Kuhusiana na mahala alipo fia kuna tafauti baina ya wana Historia kama ifuatavyo: baadhi yao wanasema alifia Hamadani na wengine husema amefia Isfahani, vyovyote vile iwavyo Ibun sina amezikwa Hamadani na kaburi lake  linapatikana hapo.

Kuathiriwa kwake na mafunzo ya Kiislamu  

Kama nilivyo sema hapo mwanzo kuwa Avicenna alijitahidi kutafsiri Quran na kujifunza Elimu ya Hadithi, hivyo basi vitu hivi vilikuwa vina mchango mkubwa katika Elimu yake  na hapa nitaashiria nukta muhimu zifuatazo:

1-Lengo la kuteremshwa  Qur’an ni kumlea na kumuongoza Mwanadamu katika masuala ya kiroho na kumfikisha Mwanadamu huyu katika saada, ukamilifu na uzima wa milele, na hapa jambo la kuzingatiwa ni kwamba ijapokua  Qur’an imeelezea kwa mapana zaidi saada ya mwanadamu lakini pia haikuacha kuashiria  masuala ya kisayansi na elimu za Tajiruba, na kuashiria kwake masuala hayo hakumaanishi kwamba  Qur’an imegeuka kuwa ni kitabu cha sayansi. kwani Elimu ya Sayansi na Tajiruba zinaweza kufikiwa na akili ya Mwanadamu pekee kwa minajili hiyo hakuna maana kusema kuwa  Qur`an  ni kitabu cha Elimu za Tajiruba. ama kuashiria kwa  Qur’an kunako masuala hayo ni kama ifuatavyo:

1.      Kumshajiisha Mwanadamu katika kumjua Mola Muumba wake

2.      Kumfanya Mwanadamu awe mchunguzi katika masuala ya Elimu ya Tajiruba

3.      Kuwashajiisha Waisilamu na wanadamu katika kutafuta Elimu katika Nyanja tafauti .kwa minajili hiyo  Qur’an si kitabu cha Tiba mpaka Wanadamu watarajie Elimu ya Tiba kutoka kwenye Qur’an la hasha sivyo hivyo kwani Elimu hizi zinaweza fikiwa kwa akili aliopewa mwanadamu.  

Ama kugusia kwake Quran katika baadhi ya masuala ya kitiba na elimu zingine za Tajiruba kama vile: utungaji wa ujauzito, alama za mikono, uponyaji wa asali,  Afya ya mwili na usalama wake, na… yote hayo ni kwaajili ya kumfanya Mwanadamu atafakari  katika alama za kuwepo Mola wake muumba na kuamsha hisia za mwanadamu huyu kunako utafiti katika masuala ya sayansi na Tajiruba.

2-Hakuna dini au kundi lolote la kiimani lilioipa kipaumbele elimu na kusisitiza kunako elimu kama ilivyo sisitiza dini ya Kiislamu, kiasi kwamba daraja ya msomi na mwanazuoni mwenye imani ni tafauti na muumini asiyekuwa na elimu, na Mwenyezi mungu anasema katika Qur’an  surat mujadalah aya 11 akisema :

یرفع الله الذین آمنوا والذین اوتواالعلم درجات

"Mwenyezi mungu atawanyanyua walioamini na wenye elimu miongoni mwenu, daraja la juu”.

na neno (elimu) katika Qur’an limekaririwa mara 80 pia neno (wenye utambuzi) na (wenye akili) limekaririwa zaidi ya mara 10 na aya zinginezo nyingi zikiwataka wanadamu wawe wenye kutafakari na kuzingatia na…

Haya yote yanaashiria  kuwa Uislamu umezingatia  zaidi na kuhimiza suala la Elimu na kutumia akili. pia upande wa hadithi za mtukufu Mtume (s.a.w) nazo zimehimiza suala la kutafuta Elimu na kutafakari kama alivyo sema mtukufu Mtume (s.a.w.w):فکرة ساعة خیر من عبادة سنة

Saa moja katika hali ya kutafakari ni bora kuliko ibada ya mwaka mmoja .

Pia anasema mtukufu Mtume (s.a.w.w): kuhudhuria katika kikao cha mwanazuoni ni bora zaidi kuliko kusindikiza majeneza Elfu moja ya waumini, kuwatembelea wagonjwa  elfu moja waumini ,… kufunga siku elfu moja... kwani mwafahamu kwamba Mungu huabudiwa  kwa Elimu.

Hivyo basi Uisilamu umesisitiza vitu viwili katika jamii ya kibinadamu navyo ni: mwanazuoni, Hakimu, na Tabibu.

Kama alivyosema Imam Swadiq (a.s) kila mji na mkoa wahitaji vitu vitatu :mwanazuoni ,hakimu wa sheria na tabibu au daktari.

Semi hizi na wito huu wa Uislamu ndio uliomfanya Ibun sina abobee katika Nyanja tofauti kwani yeye alikuwa mtaalamu wa elimu tafauti, falsafa, Erfani, Hesabu, Utabibu, na… naye ndie pekee  aliyeikosoa tiba ya Jalinusi katika kitabu alichokiandika Ibun Siina kiitwacho( Qaanun)

                                                          ***

Hivyo aviccena alizaliwa mwaka 370 A.H katika sehemu ya Balakh na kulelewa katika mazingira bora ya Kiisilamu hatimaye kujifunza Elimu za dini na baadaye kujifunza Elimu za Sayansi na Tajiruba na kupata umaarufu mkubwa duniani hapo zamani hadi sasa. na amefariki mwaka 428 A.H (Mungu amuweke  mahala pema peponi). 

non-publishable: 0
Under Review: 0
Published: 1
2638/12/30 - 10:15
|
Iran, Islamic Republic of
|
Anonymous
0
0
shukran
maoni Viewers
Name:
Email:
* Opinion: