bayyinaat

Published time: 07 ,October ,2018      20:15:54
News ID: 354

Siku chache baada ya Rais wa Marekani Bw Donald Trump kuitamkia Saudi Arabia kwamba Marekani ndio mlinzi mkubwa wa taifa hilo, Mfalme wa Saudi Arabia Bw Muhammad Bin Suleiman ameibuka na kumjibu Bw Trump.

Katika mahojiano yake na moja ya vyombo vya habari nchini Marekani Bin Suleiman amesema ni jambo la kawaida kwa marafiki kuongeleana maneno mazuri na wakati mwingine maneno mabaya.

Aidha Bin Suleiman ametumia nafasi hiyo kupinga maneno ya Trump kwa kusema kwamba kihistoria Saudi Arabia ipo katika ramani kabla hata ya uwepo wa Marekani.

".....Saudi Arabia ilikuwepo kabla ya Marekani, kuanzia mwaka 1744 nadhani ni miaka 30 kabla ya kuwepo kwa Marekani....” alisema Bin Suleiman.

Lakini pamoja na uwepo wa mrushiano wa maneno hayo bado Bin Suleiman amesifia uhusiano wake na Marekani na kusema kwamba ni moja ya uhusiano mwema hasa katika sekta ya utekelezaji ugaidi na harakati za mataifa kama Iran.


maoni Viewers
Name:
Email:
* Opinion: