bayyinaat

Published time: 07 ,October ,2018      20:18:40
News ID: 355

Taarifa iliyotolewa na mfalme wa Saudi Arabia zinasema kwamba taifa lake kwa kushirikiana na mataifa kama Urusi, wamefanikiwa kuziba pengo la uzalishaji lililokuwepo hasa baada ya Iran kuwekewa vikwazo katika uuzaji wa mafuta yake.

Akielezea namna ambavyo wamefanikiwa katika hilo Bin Suleiman amesema kuwa si tu kufanikiwa kuziba pengo hilo, bali wameweza kuzalisha mara mbili ya kiwango kilichokuwa kikizalishwa wakati Iran wapo katika soko.

Inaaminika kwamba uzalishaji mafuta ulipungua kufikia mapipa laki saba kwa siku, hali ambayo kwa sasa umeongezeka mpaka kufikia mapipa milioni moja na laki nne kwa siku.

".....Kwa maana hiyo sasa hivi kwa kila pipa moja ambalo Iran wangezalisha tunazalisha mapipa mawili...” alisema Bin Suleiman.

Pamoja na kwamba ombi la Marekani kwa Saudia kutaka kuongeza uzalishaji wa mafuta lilionekana kukataliwa ila ni kwamba chini kwa chini lilikuwa likifanyiwa kazi na hizi ni athari zake.


maoni Viewers
Name:
Email:
* Opinion: