Historia ya tiba katika Uislamu
Misingi ya tiba na udaktari ilianza pamoja na kuwepo
mwanadamu katika sayari ya dunia, na kutoka karne kwenda nyengine elimu hii
ilikuwa ikiimarika zaidi, na ulipofika Uislamu, kwa kuwa unasisitiza kutafuta
elimu na kutafakari pia uashiriaji
wake katika aya na hadithi za
tiba na udaktari, kuliwafanya Waislamu nguvu katika kufanya uchunguzi katika
suala la tiba, usalama na afya ya mwanadamu
Baada ya kumshukuru Mola muumba, na kumtakia
rehema na amani mtukufu Mtume (s.a.w.w) na ahali zake watakatifu.
Nachukua nafasi hii kuelezea kwa
ufupi historia ya tiba kisha kuangalia mtazamo wa dini ya Kiislamu kunako tiba
na afya ya mwanadamu. Swali muhimu linalopaswa kujiuliza ni kwamba elimu ya
tiba na usalama wa mwanadamu ilianza zama na kipindi gani? Pia mtazamo wa Uislamu
kuhusu tiba na suala la afya ni upi?
Ndugu msomaji naomba tushirikiane
pamoja ili kupata tija itakayotunufaisha sisi na jamii kwa ujumla katika suala
hili, Kuna khitilafu baina ya wataalamu na wana historia kunako kuanza kwa
elimu hii (tiba)! Ambapo baadhi yao wakadai kwamba mwanzilishaji wa elimu hii
ni Nabii Idrisa (a.s), huku wengine wakidai kuwa mwanzilishi wake ni: Harmas
Lul, pia wengine wakainasibisha elimu hiyo na tamaduni za Babel, Yemen, Misri,
Fars, India, Ugiriki n.k.
Wengine wakasema kuwa elimu ya
kidaktari imeanzishwa na kutambulika
kama sanaa, na baada ya karne nyingi
kupita ikapata mfumo na sura mpya na kuwa
elimu kamili.
Ndugu msomaji vyovyote iwavyo elimu
ya tiba ilikuwa sambamba na kuwepo mwanadamu
katika sayari hii (ya dunia) kwa sababu magonjwa yanaambatana na maisha ya
mwanadamu, hivyo kulikuwa kuna aina mbalimbali za tiba zilizokuwa zikitumika
katika kujiponya.
Ila ni kwamba tiba ya zama hizo ni
tofauti na sasa ukilinganisha na maendeleo ya zama zile na sasa. Hata hivyo
kuna tofauti kati ya tiba ya zama hizo na zama hizi, ukilinganisha maendeleo
yaliokuwepo zama hizo na sasa kwa sababu zama za Jalinus(201), Biqrati(277) na
Plato (428) elimu ya tiba ndipo ilipangiliwa kiufanisi na kitaalamu nawala si kwa
maana ya uanzilishi wa elimu hii, pia baada ya kudhihiri Uislamu udaktari ulipanuka
zaidi, na hii ni kwa sababu kuwa Uislamu
unasisitiza utafutaji wa elimu katika nyanja tofauti, pia katika nyanja
maalumu kama vile tiba na...
Mtume
mtukufu [s.a.w.w] anasema ; elimu ziko ya aina mbili; Elimu ya dini na
ya miili.
Maendeleo ya tiba yaliboreka kama
ifuatavyo:
a) Kutoka zama za Mtume mtukufu mpaka mwaka[133 A.H] sawa na[750 A.D]
Zama hizi za zinaambatanisha kuanzia
zama za uongozi wa Mtume mpaka zama za makhalifa wanne.
Katika zama hizi kwa sababu ya upya
wa serikali ya Kiislamu, Waislamu walishindwa hawakuipa kipaumbele kwa sababu
hiyo hakukupatikana daktari aliye bobea katika elimu ya tiba, isipokuwa kulikuwa
na watu kadhaa walikifahamika kuwa madaktari wa zama zile mfano wa
1- Shimrdel
2- Dhamad bin Thaalabah
3- Ibun Abi Ramdhah Tamimi
b) Kutoka mwaka (133A.H) mpaka mwaka
(287A.H) sawa na (900A.D)
Zama hizi zilifanyika kazi mbili nazo
ni kama zifuatazo;
1) zama za tarijama:
Zama hizi Waislamu walianza
kutarijumi vitabu vya Kigiriki, Kirumi na Kihindi ambapo aliyekuwa amesimamia
kazi hii ni Mheshimiwa Abu Zaidi Husaini bin Is-haka na mwanawe.
2) Zama za utunzi na uandishi wa
vitabu vya tiba ambapo Mheshimiwa Abu Hasan Ally bin Sahari bin Tabariy ambae
aliandika kitabu kwa jina Firdawsil Hikmah, akiwa ni mwandishi wa kwanza katika
elimu ya tiba kwa Waislamu.
c) kuanzia mwaka (287-700 A.H)
ni zama ambazo Waislamu walipiga
hatua na kuendelea katika taaluma ya tiba kiasi kwamba wasomi wa kimagharibi
walivikia kusema kuwa: muda huu ni muda wa thamani na dhahabu kwa Waislamu
kimaendeleo.
Dokta mmoja miongoni mwa madaktari wa
kimagharibi katika zama ambazo wamagharibi walikuwa katika kipindi kibaya,
kipindi ambacho Waislamu katika miji
tofauti ya kitamaduni ulimwenguni wakisonga mbele kimaendeleo ambapo Bagdad,
Damaskas, Cairo na miji mengine ambayo ilikuwa na vyuo vya kidaktari na tiba
pia kujenga mahospitali katika miji hiyo hali ambayo ikionyesha maendeleo ya
hali ya juu katika elimu ya tiba na udaktari.
Anaendelea kusema kuwa Baghdad
zilijengwa hospitali zaidi ya 60 na Cairo 33 hali ya kuwa ndani ya Ulaya
hospitali ya kwanza ilijengwa mwaka 1793 (A.D) katika mkoa wa Yuraki Uingereza.
Madaktari mashuhuri wa zama hizo
Katika zama hizo walipatikana
madaktari tofauti miongoni mwao ni:
Ibn Sina, Razi, Ahwazi, Jurjaniy, n.k
d) Zama ambazo Waislamu walishuka
kitaaluma kwa sababu zifuatazo:
1. Kukithiri kwa vita: Vita
ziliokuwa zimetokea baina ya Waislamu na uma nyingine zilipelekea kushuka kielimu
hususan katika elimu ya tiba na elimu ya kimea, kwani maadui wa Uislamu katika
vita hizo walikuwa wakichoma moto Maktaba za Waislamu, baada ya kuchukua kila
chapa ya vitabu viliokuwa humo, kitu ambacho kilikuwa ndio msingi wa kuporwa
teknolojia mbalimbali walizokuwa nazo Waislamu na kwenda jamii zingine.
2. Kukithiri kwa khitilafu za
kimadhehebu baina ya Waislamu
3 –Kukimbia kwa wanazuoni na
kwenda nchi nyengine: hali hii ilitokea kwa baadhi ya wataalamu kulazimika
kuhama katika maeneo waliokuwa kwenda nchi za kigeni, kwa maana baada ya Waislamu
kuporwa misingi ya kielimu waliokuwa nayo, pamoja na hayo maadui wa Uislamu
hakuwa wenye kuwaacha huru Waislamu hao, bali waliwajengea mazingira ambayo walifanya
baadhi ya Waislamu wachague kuhamia nchi zingine za kigeni kama unavyoona hivi
sasa kunako wataalamu wa nchi za ulimwengu wa tatu wanavyo baki katika mataifa
makubwa duniani, kwa madai mbalimbali ikiwemo urahisi wa upatikanaji wa kazi nk
4 –Kuchomwa moto maktaba za Kiislamu,
kama nilivyo bainisha katika kipengere namba mbili moja.
Sababu hizi zilipelekea Waislamu
kuporomoka kielimu na kuathiri maendeleo yao, kwa kiasi ambacho hivi sasa
kinaonekana katika uma wa Kiislamu.
Hivyo basi baada ya kuporomoka Waislamu
ndipo nchi za kimagharibi zikaanza kupamba moto na kuanzisha vitengo vya elimu
ya tiba katika karne ya 16 nchini Uingereza mkoa wa Yurak.
Hii ni ishara inayoonyesha kuchelewa kimaendeleo katika nchi za kimagharibi ukilinganisha na Waislamu katika kipindi hicho.
Misingi ya tiba na udaktari ilianza pamoja na kuwepo
mwanadamu katika sayari ya dunia, na kutoka karne kwenda nyengine elimu hii
ilikuwa ikiimarika zaidi, na ulipofika uislamu, kwa kuwa unasisitiza kutafuta
elimu na kutafakari pia uashiriaji
wake katika aya na hadithi za
tiba na udaktari, kuliwafanya Waislamu nguvu katika kufanya uchunguzi katika
suala la tiba, usalama na afya ya mwanadamu.
Waislamu waliingia katika elimu hii
hata kufanikiwa kutoa madaktari maarufu duniani, mfano wa Ibn Sina (Avicena), baada
ya hapo maadui wa Uislamu walipora elimu hii na nyinginezo kama elimu ya kemia hisabati
na kujitangaza kuwa wao ndio wenyewe, hali yakuwa si hivyo, kwa minajili
hiyo tunaweza kusema kuwa elimu ya tiba haina mwanzilishi maalumu kwani katika kila
jamii kulikuwa na aina ya tiba ambayo ilikuwa inatumika sehemu hiyo, kwani ni
jambo lisilo wezekana kuwa na taswira ya jamii bila ya tiba inayoendana na
jamii hiyo.