Kila siku Mwanadamu ajitahidi kuvumbua na
kugundua vitu tofauti ili kujua sababu ya kuwepo vitu hivyo au kutokuwepo, upeo
huo wa Mwanadamu humpelekea kujiuliza maswali mengi kunako Ulimwengu huu na
kutaka kujua ni siri gani iliyojificha ndani mwake, na kujiuliza ulimwengu
uliumbwa vipi?! Na ulichukua muda gani wa kuumbwa kwake?! na...
Kutokana na maswali hayo hadi sasa Wanazuoni wa
elimu ya Cosmology walitoa nadharia tofauti kunako kuumbwa Dunia, na nadharia
zote hizo hakuna hata moja ilionekana kuwa imeafikiwa na wote, nadharia hizo
tutaziashiria baadaye baada ya kuona mtazamo wa Quran kunako kuumbwa Dunia.
Bila shaka Quran ni Kitabu cha uongofu, na ili
kufikia katika malengo hayo ilitumia njia tofauti ili kumfahamisha Mwanadamu
kuwa Mwenyezi Mungu ni Mweza wa kila
kitu, na moja miongoni mwa njia hizo ni kutumia elimu ya Cosmology ili kumuongoza
Mwanadamu.
Quran haijazungumzia moja kwa moja jinsi ya
kuumbwa Dunia ila imeashiria tu mwanzo wa Dunia jinsi ulivyo kuwa, na Aya
mbili ndizo zimeashiria suala hili na kutafsiriwa
tofauti ila madhumuni yao ni mamoja, na Aya hizo ni:
1-
ثُمَّ اسْتَوَى إِلَى السَّمَاءِ وَهِيَ دُخَانٌ...
"Kisha aliumba mbingu, na ilhali zilikuwa
moshi...” Quran 41/11.
Na Neno(دُخَانٌ) katika Aya hii linamaanisha Moshi au Gesi na kuwa sambamba na maana
Kilugha, ama Neno(السَّمَاء)
linamaanisha anga au kila kilichokua juu, na Neno(اسْتَوَى)linamaanisha mapumziko, kuwa sawa vitu
viwili na kumiliki kitu.
2-
أَوَلَمْ يَرَ الَّذِينَ كَفَرُوا أَنَّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ
كَانَتَا رَتْقًا فَفَتَقْنَاهُمَا وَجَعَلْنَا مِنَ الْمَاءِ كُلَّ شَيْءٍ حَيٍّ أَفَلَا
يُؤْمِنُونَ.
"Je! walio kufuru hawakuona kwamba mbingu
na ardhi zilikuwa zimeambatana, kisha Sisi tukaziachanisha? Na tukaumba kwa
maji kila kiumbe kilicho hai? Basi je, hawaamini? ”Quran
21/30.
Na Neno(رَتْقًا) lina maana ya kuambatana na
kuambatanisha, na Neno(فتَقاً) maana
yake ni kuachana na kuachanisha.
Dhahiri ya Aya mbili hizi yaonyesha kuwa kabla
ya kuumbwa Dunia kulikuwepo Gesi, na Gesi hiyo ilisababisha Mbingu na Ardhi
kuambatana ila Mwenyezi Mungu aliziachanisha.
Ayatullah Makarim Shirazi: katika kufafanua sentensi
hii kasema "Kisha aliumba mbingu, na ilhali zilikuwa moshi...” ni
ishara ya kuwa mwanzo wa Dunia ilikuwa
ni mkusanyiko wa Gesi, na maneno haya ni sambamba na uhakiki uliofanywa hivi
karibuni kunako chanzo cha kuwepo Dunia, kuthibiti hilo ni kutokea Sayari
nyingi kupitia mkusanyiko wa Gesi.
Kauli tatu za Wafasiri wa Quran kunako Aya hii:
1-Kushikana Mbingu na Ardhi ni ishara ya kuanza
kuumbwa Dunia, kulingana na nadharia za Wanazuoni ni kuwa Dunia ni mkusanyiko
wa Gesi na Mvuke uliokusanyika baada ya miripuko ya anga, na kulingana na
miripuko hiyo ikakusanyika Gesi sehemu mbalimbali na kusababisha kutokea Sayari
tofauti Sayari ya Dunia na nyinginezo.
2-Kushikana Mbingu na Ardhi maana yake ni kuwa
sawa Mbingu na Ardhi, ama baada ya kupita muda kadhaa ikaachana Mbingu na Ardhi
na kuanza kuota mimea na kuwepo viumbe tofauti katika Mbingu na Ardhi.
3-Kushikana Mbingu na Ardhi inamaanisha
kutonyesha mvua, na Kushikana Ardhi na Mbingu ni kutokuwa mimea katika Ardhi
katika muda ule, ama Mwenyezi Mungu kwa uwezo wake alishusha mvua na akaotesha
mimea katika Ardhi.
Pia Wanazuoni na Maulama waitakidi kuwa Gesi au
moshi ilikua hatua ya kwanza ya kuumbwa Dunia kwani hapo kabla Mbingu na Ardhi
zilikuwa zikishikana na baadaye zikaachana.
Baadhi ya Nadharia za Wanazuoni wa elimu ya
Cosmology:
1-Dunia ni athari ya mlipuko mkubwa uliotokea
kabla ya miaka milioni 20 iliopita, baada ya mlipuko huo Gesi na Moshi
ulijikusanya sehemu moja na kuanza kuweka kitu kama nukta ndogo na baada ya muda
ikawa nukta ile ikikua miaka hadi miaka na hatimaye kutokea Sayari ya Dunia hii
tuliyomo, nadharia hii ni ya mwaka 1900.
2-Dunia ni athari ya miripuko midogo iliokuwa
ikitokea na kukusanyika sehemu moja, baada ya miaka kadhaa kuwa Sayari ya
Dunia. Pia kuna nadharia nyingi kunako kuumbwa Dunia ila tu muda hutoshelezi
kutaja zote.
Kwa mantiki hii kama tulivyo tangulia kusema
hapo kabla, Quran haijazungumzia moja kwa moja jinsi ya kuumbwa Dunia, ila tu
iliashiria mwanzo wa Dunia ulivyo kuwa, kulinga na ishara hizo za Quran
kukatolewa tija kutokana na nadharia za Wanazuoni, na nadharia iliokuwa karibu
na ishara ya Quran ni ile nadharia ya Wanazuoni inayosema kuwa; Dunia ni athari
ya mripuko mkubwa uliotokea kabla ya miaka milioni 20 iliopita. Kwa upande mwingine
kulingana na wingi wa nadharia kunako
kuumbwa Dunia kwa Wanazuoni wa elimu ya Cosmology nadharia zilizokuwa kinyume
na ishara ya Quran haziwezi kutabikishwa na kuthibitisha kuumbwa Dunia kwa kuwa
kwake kinyume na ishara hizo.
Hii ndio Quran mbayo ni muujiza wa milele isio
na kasoro ndani yake, Quran imezungumzia mambo mengi ambapo hapo kabla Wanazuoni
walikua hawaelewi Quran inamaanisha nini, baada ya kupita miaka ndio Wanazuoni
na Wagunduzi walielewa Quran inamaanisha nini.
Na Sh Khamis Sadiki