Jamii
Familia
Mwenyezi Mungu anasema katika kitabu chake kitukufu;
وَمِنْ آيَاتِهِ أَنْ خَلَقَ لَكُمْ مِنْ أَنْفُسِكُمْ أَزْوَاجًا لِتَسْكُنُوا إِلَيْهَا وَجَعَلَ بَيْنَكُمْ مَوَدَّةً وَرَحْمَةً إِنَّ فِي
ذَلِكَ لَآيَاتٍ لِقَوْمٍ يَتَفَكَّرُونَ
Na katika ishara zake ni kuwa amekuumbieni wake zenu kutokana na nafsi zenu ili mpate utulivu kwao. Naye amejaalia mapenzi na huruma baina yenu. Hakika katika haya bila ya shaka zipo ishara kwa watu wanao fikiri.
Bwana Mtume naye pia (s.a.w.a) anasema:
النِّکَاحُ سُنَّتِی فَمَنْ رَغِبَ عَنْ سُنَّتِی فَلَیْسَ مِنِّی
“Kuoa ni moja katika sunna zangu na atakaye acha sunna yangu sio miongoni mwangu.”
3. Ukomavu wa kiuchumi
Ukomavu wa kiuchumi inamaanisha kuwa na uwezo na ujuzi wa kutafuta pesa, kuhifadhi pesa hizo, usimamizi mzuri wa pesa hizo na uendeshaji mzuri wa gharama za maisha. Katika baadhi za tamaduni, mara nyingi inaonekana kwamba jukumu la kusaka fedha linapaswa kuwa la wanaume na jukumu la kusimamia gharama za maisha ni la wanaume na wanawake kwa pamoja.