bayyinaat

Published time: 21 ,February ,2017      22:12:10
je, vazi la hijabu katika dini ya Kiislamu lina faida yoyote?
News ID: 19


Ndugu Mwislamu Hijabu ni stara adhimu kwa Mwanamke na huhesabika kuwa ni miongoni mwa hukumu za kisheria ambazo ni za dharura katika dini tukufu ya Kiislam.

Mwenyezi Mungu amesema:

«يا أَيُّهَا النَّبِىُّ قُلْ لِأَزْواجِكَ وَ بَناتِكَ وَ نِساءِ الْمُؤْمِنِينَ يُدْنِينَ عَلَيْهِنَّ مِنْ جَلَابِيبِهِنَّ ذلِكَ أَدْنى أَنْ يُعْرَفْنَ فَلا يُؤْذَيْنَ وَ كانَ اللَّهُ غَفُوراً رَحِيماً». 

"Ewe Nabii! Waambie wake zako, na binti zako, na wake za Waumini wajiteremshie nguo zao. Hivyo ni karibu zaidi kuweza kutambulikana wasiudhiwe. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu”. (Suratul Ahzaab/59).

Pia ni muhimu mno kuashiria nukta kadhaa zinazohusiana na Umuhimu na falsafa ya vazi hilo ambazo ni hizi zifuatazo:

1. Kuheshimu vazi hili imepelekea kupungua maovu katika jamii kwa wenye matamanio ya haraka pindi ionekanapo shepu ya mwili wa mwanamke asiye jisitiri vizuri.

2. Hijabu inalinda heshima ya mwanamke, ambapo wakati mwingine hijabu husaidia wanaume kumiliki hisia zao, kwa matakwa yao wenyewe pindi mwanamke anapojisitiri.

Amesema Mtume Muhammad (saw):

النَّظر سهمٌ مسمومٌ من سهام ابليس فمن تركها خوفاً من اللَّه اعطاه اللَّه ايماناً يجد حلاوته فى قلبه

"Kutazama (mwili wa Mwanamke asiyejisitiri) ni mtego katika mitego ya Ibilisi, hivyo yeyote atakayeacha kutazama Miili ya wanawake wasiojisitiri, basi Mwenyezi Mungu atampa imani thabiti ambayo atapata ladha ya imani hiyo ndani ya moyo wake”.

Ndugu msomaji: Namna ya ushonaji nguo, una mchango mkubwa katika vazi la kumstiri Mwanamke. Mavazi mepesi, mavazi ya yakubana, ni makosa.

Hivyo, wadhifa wa Uislamu ni kumlinda Mwanamke kikamilifu. kwa lengo la kuzuia kusisimua hisia za Wanaume wenye matamanio ya haraka, na ili nguzo ya mwanadamu pamoja na nidhamu ya dini ibaki kuwa madhubuti.

maoni Viewers
Name:
Email:
* Opinion: