DHULMA KWA MWANAMKE KABLA
YA UISLAMU
Dhulma kwa mwanamke katika ulimwengu wa kabla
ya Uislamu imegawanyika katika vipindi vya aina mbili:
1.
kipindi cha uhayawani ambayo
mwanamke hakutambulika kama mwanadamu na hatimaye kuamiliana naye kwa ukali wa
hali ya juu. Na miongoni mwa mikingamo mikubwa iliyomsibu mwanamke, ilikuwa ni
mwanaume kumuuza au kumkodisha kwa mwanaume mwingine.
2.
Kipindi cha tamaduni za kale za Kigiriki,
Misri, Roma pamoja na tamaduni za Iran kwa mwanamke hazikumteulia haki yoyote
ile ya kimsingi wala ya kijamii, naye alitambulika kuwa ni mfuasi wa mwanamke
(Yaani; Kila aliamualo mwanaume juu yake basi yeye hufuata na kutii matakwa ya
mwanaume).
MWANAMKE KATIKA BARA LA ULAYA:
MWANAMKE KATIKA MILA NA TAMADUNI ZA KALE ZA
UGIRIKI NA ROMA:
Katika tamaduni za Ugiriki
mwanamke alihesabika kuwa ni bidhaa ya kibiashara kama bidhaa nyingine, ambaye
alikuwa akiuzwa na kununuliwa masokoni, bila kujali shakhsiya yake wala haki
zake za kijamii, pia baada ya kufariki mumewe (kwa mujibu wa itikadi zao
potovu) ni kwamba alipoteza haki ya kuendelea kuishi. Vilevile mwanaume alikuwa
ni mwenye uwezo wa kumkodisha mwanamke kwa mwanaume yeyote ule amtakaye au
kumzawadia rafiki yake.
Katika tamaduni za Roma kabla ya
kuzaliwa Nabii Issa (a.s) ni kwamba, mwanamke na msichana walitumikishwa kama
watumishi bila kujali shakhsiya katika jamii, pia walifananishwa na wanyama. Na
walikuwa wakiuzwa na kununuliwa mfano wa bidhaa za kibiashara, alinyimwa haki
zake za kijamii. Kama vile alivyokuwa hana haki ya kumrithi mzazi wake au
kumiliki kitu chochote kile.
Pia mwanaume alikuwa na haki ya
kumkagua mwanamke (kwa mujibu wa itikadi zao potovu) na vilevile alikuwa na uwezo wa kumhukumu kifo kwa sababu
ya kosa lake.
URUSI:
Katika tamaduni za kale za Urusi
ilikuwa kwamba Baba alipokuwa akimuoza binti yake, anampeleka ukweni kwake,
kisha Bi harusi alipokuwa akifikishwa kwa ukweni, basi Baba anatoa hukumu ya
kupigwa bakora na Mumewe, ili ifahamike katika akili za wanawake ya kwamba;
Iwapo mwanamke atakuwa ukweni atambue kuwa yeye kupigwa na mumewe ni ada na
desturi ambayo ni lazima aifahamu pindi atakapokuwa ukweni.
Vile vile katika tamaduni za kale
za Yugoslavia pamoja na Serbia ilikuwa kwamba (Mwanamke alihesabika kuwa ni
fungu katika mafungu ya ngawira za kivita) pia wanawake kuporwa na kuibiwa ni
jambo ambalo liliendelea kuenea hadi karne iliyopita.
MWANAMKE KATIKA MTAZAMO WA DINI ZA
KIYAHUDI NA KIKRISTO:
Kwa mujibu wa dini ya Kiyahudi, ni
mfano wa zile itikadi potovu za Waarabu kabla ya Uislamu, kwamba; Anapozaliwa
mtoto wa kike basi humhesabu kuwa ni nuksi kwa baba, pia Mama huyo alijifungua
mtoto wa kike naye pia alihesabika kuwa ni nuksi kwa muda wa siku kumi tano
hadi sabini. Hivyo mwanamke (Kwa mujibu wa dini hizo) alikuwa ni fungu katika
mafungu ya urithi wa Baba wa familia.
Vilevile katika jamii za Kikristo
mfano; Italia na Hispania, baada ya midahalo mingi iliyojiri baina yao
ikapelekea kuitikadi ya kwamba katika wanawake
wote ulimwenguni Mariam (a.s) ni mwanamke pekee aliyekamilika na mwenye roho ya
milele, na kwamba wanawake baki wamekosa sifa ya uanadamu katika jamii, na
kuongezea hilo ni kwamba hana roho ya milele, hivyo huhesabika kuwa ni jahanamu
ililokuwepo baina ya mwanadamu na mnyama.
Kwa msingi huu ni kwamba, wako
baadhi huamini ya kwamba ni bora baada ya kifo cha mwanaume, mkewe naye asibaki
hai, yaani azikwe pamoja naye akiwa hai, kwani iwapo ataendea kuishi basi hana
haki ya kuolewa tena na mwanaume mwingine.
MISEMO YA WAMAGHARIBI KUHUSIANA NA
MWANAMKE:
Katika wa watu wa magharibi imeenea
misemo ambayo ni ya kustaajabisha mno kuhusiana na mwanamke. Ambayo miongoni
mwake ni hii ifuatayo:
v
Mwanamke, ni kiumbe mfano wa
kizingiti na mpungufu wa akili.
v
Mwanamke, ni kiumbe wa duni
mithili ya hayawani ambaye humaliza matamanio ya mwanaume.
Waingereza:
v
Mwanaume anapomchukua mwanamke ni
mfano wa mtu anayelea nyani.
v
Wanawake ni mikia ya Shetani.
Wajerumani:
v
Mwanaume ni mwenye maumbile ya
Malaika, moyo wake ni wa nyoka na hisia zake ni mfano wa punda.
v
Matendo yote ya Shetani
huyakabidhi kwa wanawake kuyatekeleza.
Wagiriki:
v
Mambo matatu ni mkosi: Mwanamke,
moto pamoja na tufani (Kimbunga).
Na misemo mingine mingi zaidi ya hiyo
inayoshusha hadhi pamoja na shakhsiya ya mwanamke na vilevile kumnyima haki
zake za kisheria.