bayyinaat

Published time: 27 ,February ,2018      18:18:53
News ID: 246
Umoja wa Mataifa kwa mara nyingine tena umeelezea wasiwasi ulionao0 kuhusiana na hali inayotawa katika nchi ya Burundi.
Mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Burundi ameliambia Baraza la Usalama la umoja huo kwamba mgogoro wa nchi hiyo unatia wasiwasi.
Michel Kafando amesema kuwa, nafasi ya Umoja wa Mataifa katika mgogoro wa Burundi si kuingilia wala kupendelea upande wowote na kwamba Umoja wa Afrika unapaswa kudumisha juhudi za upatanishi nchini humo.
Burundi ilitumbukia katika machafuko ya ndani mwishoni mwa mwezi Aprili mwaka 2015 baada ya chama tawala cha CNDD-FDD kumuidhinisha Rais Pierre Nkurunziza kugombea urais katika uchaguzi mkuu uliopita kwa mara ya tatu mfululizo kinyume na makubaliano ya Arusha.
Tangu wakati huo mamia ya watu wameuawa na maelfu wamelazimika kukimbilia katika nchi jirani kutokana na ghasia na machafuko ya ndani. 
Mwezi Novemba mwaka uliopita majaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu waliruhusu kuanzishwa uchunguzi kuhusu ukatili na jinai zinazofanywa dhidi ya binadamu nchini Burundi katika kipindi cha kati ya mwaka 2015 na 2017. Jinai hizo ni pamoja na mauaji, ubakaji, ukatili na mateso yaliyoanza mwaka 2015 baada ya Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza kutangaza nia yake ya kugombea kiti hicho kwa muhula wa tatu mfululizo.

maoni Viewers
Name:
Email:
* Opinion: