Umuhimu wa Sala katika kauli za Mtume(s.a.w.w).
- Sala
humzuia mwanadamu kutenda maovu.
- Sala
ni miiraji ya Muumini.
- Sala
ni chanzo cha kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu.
- Sala
ni amali bora inayomkurubisha mwanadamu kwa Mola wake.
- Sala
ni nguzo ya dini.
- Sala
ni nuru ya Muumini.
- Sala
ni ngao ya vitimbi vya Sheitani.
- Sala
ni ufunguo ya pepo.
- Sala
ni gharama ya pepo.
- Sala
ni bora kuliko Hijja.
- Sala
ni amali bora mno mbele ya Mwenyezi Mungu.
- Sala
ni nuru ya macho yangu (Mtume (s.a.w.w)).
- Kupitia
sala huridhia Mwenyezi Mungu amali za Muumini.
- Sala
ni sera za Manabii.
- Sala
ni ripoti nzuri waipendayo Malaika.
- Sala
ni taa ya moyo wa Muumini.
- Kupitia
sala hujibiwa dua za Muumini.
- Sala
ni mnong’ono pamoja na Mwenyezi Mungu.
- Sala
hushusha rehema za Mwenyezi Mungu.
- Sala
ni nuru ya uso wa Muumini.
- Sala
ni Baraka kwa taifa.
- Sala
huzidisha riziki ya mja wa Mwenyezi Mungu.
- Sala
ni silaha ya Muumini kwa adui.
- Sala
ni kafara ya madhambi.
- Sala
ni mahari ya Huurul-Ain.
- Sala
ni kibali cha kuvuka daraja la sirat.
- Sala
ni nuru na kivuli siku ya kiama.
- Sala
ni taji ya kichwani ya muumini siku ya kiyama.
- Sala
ni taa la kaburini.
- Sala
ni uokovu wa mwili kutokana na moto wa jahanamu.
- Sala
ni maandalizi ya Muumini akhera.
- Sala
ni tegemeo bora kaburini.
- Sala
ni ponyo baina ya mtu na Malaika wa mauti.
- Sala
humuepusha Muumini na moto wa jahanamu.
- Sala
ni jawabu la Munkar na Nakiir kaburini.
- Sala
ni ripoti ya kukubaliwa amali za Muumini.
- Sala
ni utulivu wa mwili wa Muumini.
- Sala
ni swali la kwanza siku ya kiyama.
- Sala
ni kafara ya amali isiyo kubaliwa kwa Mwenyezi Mungu.
- Sala
ni amali bora zaidi baada ya mja kumfahamu Mola wake Mlezi.[1]
SALA
Kwa
itikadi ya kila Mwislamu ni kwamba Sala
ni nguzo ya dini, na Sala ni ngazi ya mja kumfikia Mola wake. Mtu anapokuwa
ameacha Sala huwa anakuwa amekata mawasiliano baina yake yeye na Mola wake, kwa
ajili hiyo zimepokelewa hadithi nyingi kutoka kwa Mtume (s.a.w.w) na Ahlul-Baiti ya kwamba: tofauti baina ya Uislamu na
ukafiri ni; kuacha Sala au kujivua Uislamu.
KUMBUKUMBU
Siku
ambayo Mfalme wa Iran alipotoroka nchini Iran, Imamu aliuhutubia ulimwengu
alipokuwa mjini Paris huku akizungukwa na waandishi wa habari na stesheni mbalimbali
za televisheni.
Siku
hiyo, ilikuwa ni siku nzuri katika historia ya Iran, pia ujumbe ule wa Imamu
Khomeini ulikuwa ni ujumbe muhimu mno kwa walimwengu.
Wakati
huo Imamu alikuwa amekaa kwenye kiti akitoa hotuba kwa umma, punde akamuuliza
mwanae aliyekuwa pembezoni mwake: Je! Muda wa Sala haujafika?, akamjibu kuwa:
Ndio muda wa Sala umewadia.
Imamu
ambaye alikuwa akihutubia dunia alikatiza maongezi yake na kuelekea kusali.
Waandishi wote wa habari walitahayari sana na kujiuliza kwa nini ghafla amekatiza
hotuba yake muhimu?. Wakaambiwa kuwa: ((Imamu huwa ana maongezi na Mola wake
kila unapofikia muda wa Sala, na muda huo unakuwa si kwa ajili ya watu)).