AKILI NI NINI?
Akili ni chombo alichopewa mwanadamu ili
kutofautisha kizuri na kibaya, halali na haramu, mubaha na makuruh, na kwa
sababu hii mwanadamu akawa bora kuliko mnyama.
Je Mwenyezi Mungu amezungumziaje akili? Anasema
" na ule mfano tumewapigia watu, na hawauelewi isipokuwa wale wenye akili”
Nahl:12.
”Hivyohivyo
tunazifafanua aya zetu kwa watu wenye akili” Rum;27.
"Lau
tungekuwa ni wenye kusikia au wenye akili, tusingekuwa watu wa motoni” Mulk;
10.
Aya
zote hizo hapo juu zinazungumzia uzito
wa akili, akili ndiyo ambayo inakuongoza katika kutenda jambo lolote lile. mwenye akili iliyosalimika
atafanya matendo mazuri na yenye kuridhisha na mwenye akili mbayo ina kasoro,
atafanya matendo mabaya na yenye kuchukiza.
Bwana
Mtume (s.a.w.w) aliulizwa na masahaba zake; ni nini hiyo akili? akawajibu; "ni
kutenda jambo kwa kumtii Mwenyezi Mungu, na watendao matendo mema hao ndiyo
wenye akili”.
Bwana
Mtume( s.a.w.w) alimwambia Ali(a.s); "Ewe Ali! pindi waja wakijikurubisha kwa
muumba wao kwa mema, basi wewe jikurubishe kwa muumba wako kwa akili
utawashinda, hakika sisi Mitume tunazungumza na watu kwa kiasi cha akili zao”.
Kwa
hivyo hapo tunaona umuhimu wapekee wa akili aliyopewa mwanadamu, pia ametakiwa
aitumie akili hiyo katika kupambanua mambo kwa kutumia akili ,katika mafunzo
anayotupa Bwana Mtume (s.a.w.w) kuhusu akili, anasema: "hakugawa Mwenyezi
Mungu kwa waja wake kitu kilicho bora zaidi kuliko akili, usingizi wa mtu
mwenye akili ni bora zaidi kuliko kukesha kwa mtu mjinga (asiye na akili)".
Na
hakutumwa nabii yoyote wala mjumbe yoyote mpaka awe amekamilika kiakili, na
akili yake iwe ni bora kuliko akili za watu wote, na huenda katika watu hao
akawepo mtu mwenye kujitahidi zaidi lakini hawezi kumshinda huyo Mtume”.
Hadithi
hii yaonyesha kuwa mtu mwenye akili hata kulala kwake ni bora kuliko kukesha
kwa mtu asiye na akili, kwani kukesha huko hakuna maana yoyote ikiwa anayoyafanya
hayaendani na akili iliyosalimika, mfano hivi leo utawaona watu wanashinda au wanakesha katika ngoma, disko, taarabu,
drafti, karata n.k .na wengine wakitoa fedha nyingi kwa ajili ya mikesha hiyo je
hiyo ni sawa kwa mwenye akili?
Imepokewa
kutoka kwa Bwana Mtume (s.a.w.w) yeye alimwambia mmoja wa masahaba wake aliyeitwa
Uwaymir "Ewe Uwaymir zidisha akili, utazidi kuwa karibu na mola wako na kuwa na
akili ni utajiri!! Uwaymir akasema; nakufidia baba yangu na mama yangu, nifanye
nini kwa hiyo akili? Bwana Mtume (s.a.w.w)
akasema "jiepushe na haramu za Mwenyezi Mungu, na tekeleza faradhi za mwenyezi
mungu utakuwa ni mwenye akili! Kisha tenda matendo yaliyo mema utawazidi waliyopo
duniani kwa akili, na utazidi kuwa karibu kwa mola wako kwa utukufu”
VIPI
TUTAHIFADHI AKILI ZETU ILI ZIBAKIE SALAMA?
Tunahimizwa
tujiepushe na mambo ya haramu yaliyokatazwa na Mwenyezi Mungu, na tutekeleze
ibada zetu kwa amri ya mwenyezi mungu ndipo utakuwa mwenye akili, hapa
tunamuomba msomaji wetu awe makini
kuelewa kinacho kusudiwa. Tunapozungumzia akili na mtu mwenye akili, na kusema
kwamba fulani ana akili na fulani hana akili, tunakusudia utendaji kazi wa
akili ya kila mtu, kwani akili ni kifaa ambacho kila mtu amepewa na Mwenyezi
Mungu, kama hadithi inavyosema:
أخبرنا أبوجعفر محمد بن يعقوب
قال: حدثني عدة من أصحابنا منهم محمد بن يحيى العطار عن أحمد بن محمد، عن الحسن بن
محبوب، عن العلاء بن رزين، عن محمد بن مسلم، عن أبي جعفر عليه السلام قال: لما خلق
الله العقل استنطقه ثم قال له: أقبل فأقبل ثم قال له: أدبر فأدبر ثم قال: وعزتي
وجلالي ما خلقت خلقا هو أحب إليّ منك ولا أكملتك إلا فيمن احب، أما إني إياك آمر،
وإياك أنهى وإياك اعاقب، وإياك اثيب
Wapokezi
wa hadithi hii wanaishia kwa Abu Jafari ambaye ni Imam Baqir anasema: pindi
Mwenyezi Mungu alipoiumba akili, alizungumza nayo, kisha akaiambia nenda mbele
ikaenda ,kisha akaiambia rudi nyuma ikarudi, na hapo Mwenyezi Mungu akasema, kwa
nguvu zangu na utukufu wangu sikuumba kiumbe ambaye nampenda sana kuliko wewe
na wala sikukuumba na kukukamilisha isipokuwa ni kwa yale ninayoyapenda, ama
kwako nitaamrisha ,na kwako nitakataza, na kwako nitaadhibu, na kwako nitatoa
thawabu.
Na
kifaa hiki Mwenyezi Mungu akakiweka ndani ya kila mwanadamu ili kifanye kazi na
sasa tukiwa tunajibu swali letu la vipi tutahifadhi akili ili ibakie salama, na
ibaki inafanya kazi, tunamaanisha kwamba kuna baadhi ya matendo, ambayo
mwanadamu anayafanya ambayo yanapelekea kudhoofika nguvu ya akili au kupotea
kabisa, hapa ndipo tutasema fulani akili yake haiko sawa au fulani hana akili. na
wakati mwingine tunazungumzia akili tukiwa tunakusudia elimu, na tunafanya
hivyo kwa sababu makazi ya elimu ni ndani ya akili, kwa hiyo tukisema kwamba
kuna mambo yakifanywa yatadhoofisha akili, iwe akili kwa maana ya akili ya
asili itadhoofika, au iwe akili ambayo ni elimu na ambaye inakaa ndani ya akili
kama akili yenyewe, vyote vitadhoofika. (yaani akili na elimu inayokaa ndani ya
akili, ambayo wakati mwingine inaitwa akili, na hii ndiyo akili iliyokamilika).
Mtume
(s.a.w.w) anasema :akili ina vigawanyo vitatu, ambaye atakuwa navyo akili yake
imekamilika na ambaye hana vigawanyo vivyo hana akili.1-kuwa na maarifa sahihi
juu ya Mwenyezi Mungu,2-kumtii inavyotakiwa,3-na kuwa na subira isiokatika juu
ya yale anayoyaamrisha, tukitimiza haya akili zetu zitabakia salama.
وقال نبي الرحمة (ص) إذا أذنب العبد ذنبا فارقه
عقل لا يعود إليه أبدا
Mtume (s.a.w.w) anasema atakapofanya mja dhambi akili inajitenga
naye na hairudi abadani.
Bwana
Mtume (s.a.w.w) amesema; "kichwa chenye akili baada ya imani na Mwenyezi Mungu kinapendana
na watu” na kupendana na watu ni dalili ya kuwa na akili nzuri na timamu.