bayyinaat

Published time: 05 ,March ,2017      22:19:57
Ni siku ya Ijumaa ya tarehe 17 mnamo mwaka ambao umejulikana kama mwaka wa tembo kutokana na tukio maarufu lililotokea mwaka huo......
News ID: 31

Mtume Muhammad (saww)

ni wa kwanza katika ambao wanatengeneza idadi ya maasumina 14 watakatifu, kama ambavyo pia yeye ni mtume wa mwisho katika mitume ya mwenyezi mungu swt.

Jina lake ni Muhammad.

Baba yake ni Abdullahi.

Mama yake ni Amina binti Wahab.

Babu yake ni Abdul Mutalib.

Tarehe ya kuzaliwa ni 17 Rabiul awwal (mfungo sita) katika mji mtukufu wa Makka.

Tarehe ya kufariki ni 28 Safar (mfungo tano) baada ya kuugua kwa muda mrefu kutokana na sumu aliyopewa na mwanamke wa Kiyahudi.

Mahala alipozikwa ni mji mtukufu wa Madina.

Idadi ya watoto ni 6 watatu wakiwa wa kike na watatu wakiwa ni wa kiume.

 

Mazazi yake matukufu

Ni siku ya Ijumaa ya tarehe 17 mnamo mwaka ambao umejulikana kama mwaka wa tembo kutokana na tukio maarufu lililotokea mwaka huo, ambapo nuru ya Mtukufu Mtume (saww) iliweza kudhihiri katika ulimwengu huu. Na ili kuonyesha kwamba haikuwa ni jambo la kawaida ndio maana tunaambiwa kwamba wakati wa kuzaliwa kwake kuna baadhi ya matukio ambayo yalitokea siku ile, na baadhi ya matukio hayo ni kama:

1.      Kuanguka kwa masanamu ambayo yalikuwa yakiabudiwa kwa miaka mingi.

2.      Moto wa majusi ambao ulikuwa ukiabudiwa nao ulizimika kwa uzito wa mazazi yake.

3.      Kuwaka kwa nuru ambayo iliangaza sehemu kubwa mno ya Arabuni.

Na matukio mengi sana ambayo historia ya mazazi ya Mtume imeyabainisha, lakini hayo yote yakiwa ni katika kuonyesha ishara ya kwamba mtu huyu aliyezaliwa hakuwa mtu wa kawaida bali alikuwa na jambo mahususi lililopelekea kutokea kwa matukio haya.

Abuu talib (baba mdogo wa mtukufu Mtume)

Huwezi kuzungumzia shahsia muhimu katika maisha ya bwana mtume saww, bila ya kutaja shahsia hii, baba mdogo na mlinzi mkubwa wa bwana Mtume saww, na hii ni kutokana na duru yake kubwa aliyokuwa nayo katika kuhakikisha kwamba mtukufu Mtume hapatwi na madhara yeyote kutoka kwa watu wa Maka. Na si tu kwamba alikuwa ni mwenye kumtetea basi, bali alikuwa ni mtu ambaye pia mwenye imani juu ya utume wa mtukufu Mtume saww kama ambavyo vitabu vya historia vinanukuu hivyo.

 

 

Kuhama kwake

Miongoni mwa matukio muhimu katika maisha ya bwana mtume ni tukio zima la kuhama kwake Maka na kuelekea Madina. Na kuhama huku bila shaka kulikuwa na sababu zilizopelekea kutokea kwake, kwani ni lazima tutambue kwamba mnamo mwaka wa kumi, mwaka ambao mtukufu Mtume aliuita kwamba ni mwaka wa huzuni kutokana na kuambatana kwa misiba miwili mizito, msiba wa baba yake mdogo na msiba wa mke wake kipenzi bibi Khadija (ra), hivyo hata wale ambao walikuwa wanashindwa kumuudhi mtukufu mtume kutokana na uhai wa watu hawa, sasa walipata nafasi ya kuweza kumuudhi.

Hivyo Mtume akawa hana namna zaidi ya kuhama na kwenda mji mwingine ambapo atapata hifadhi na kutoudhiwa. Ndipo alipojaribu kwenda mji maarufu wa Taif, lakini kutokana na kutokubalika na watu wa mji ule na si tu kutokukubalika bali hata kuudhiwa na kujeruhiwa pia, aliamua kupanga safari ya kuhamia mji wa Madina ambapo alipata watu wa kumnusuru yeye pamoja na masahaba zake, na kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu harakati za kufikisha ujumbe ziliweza kuendelea.

 

 

 

maoni Viewers
Name:
Email:
* Opinion: