bayyinaat

Published time: 08 ,March ,2017      17:44:37
Imam Mahdi (as) ni Imam wa kumi na mbili wa Mashia, na Baba yake alikuwa anaitwa Imam Hassan Askarii(a.s). Imam wetu Mutkufu alizaliwa katika siku ya Ijumaa Mwaka wa 255 katika Mji wa Samaraو na Jina la Imam Mahdi(a.s) ni kama Jina la Babu yake Mtume (s.a.w.w)........
News ID: 49

IMAMU MAHDI (as)

Katika ukurasa huu ningependa kumzungumzia Imam wa zama hizi ambae ni maarufu kwa Jina la Imam Mahdi (a.s). Pia ningependa kumzunguzia Baba yake pamoja na Mama yake kwa ujumla.

KUZALIWA KWAKE

Imam Mahdi (as) ni Imam wa kumi na mbili wa Mashia, na Baba yake alikuwa anaitwa Imam Hassan Askarii(a.s). Imam wetu Mutkufu alizaliwa katika siku ya Ijumaa Mwaka wa 255 katika Mji wa Samar`ra na Jina la Imam Mahdi(a.s) ni kama Jina la Babu yake Mtume(s.a.w.w).

Wanahistoria wanasema; Jina hilo la hadharati alipewa na Mtume Mtukufu (s.a.w.w) , kutokana na kufanana kwa Majina hayo ni dalili tosha ya kwamba kudhihiri kwa Mtume ni kuwaondoa watu katika dimbwi la ujinga, na kwa kudhihiri kwa Imam Mahdi (a.s) ni kuwatoa watu katika giza walilo kuwemo.

Lakabu za hadharati zimegawanyika katika sehemu kuu zifuatazo:

Qaaim, Muntadhar, Hujjat, baqiatu llah, Wali Asri, Swahiba Zaman na Mahdi. Haya Majina mawili ya mwisho ndio Majina maarufu sana katika jamii.

Mama yake Imam Mahdi (as)  alikuwa akiitwa Nargisi, wahakiki wamethibitisha ya kwamba Mama huyo alikuwa ni Mtumwa.

KUZALIWA KWAKE KWA UFICHO

Imam Hassan Askarii (as) kipindi alipokuwa kiongozi, watu wa Banii Abbasi walipatwa na wasiwasi mkubwa  kutokana na habari zilizotoka kwa Mtume (saw) na Maimamu (as) kuhusu kuzaliwa Mtoto wa Imam Askarii (as), ambaye atakayekuja  kuangamiza dhuluma, na kuweka Uadilifu. Imam Askarii alikuwa akichunguzwa sana mpaka atakapozaliwa Mtoto huyo. Kutokana na sababu hiyo kukawa kuzaliwa kwake ni kwa maficho na hakuna watu waliotambua chochote kile kinachoendelea.

Imam Ridha(as) anasema: "moja ya sifa  ya Imam Mahdi ni kuzaliwa kwake kwa maficho.” Na pia hadithi nyingi zinaeleza ya kwamba Imam anafanana na Hadharat Ibrahim (as) na Hadharat Mussa(as).

ZAMA ALIZOISHI IMAM MAHDI

Zama alizoishi Imam zimegawanyika katika sehemu kuu tatu; 1- Zama ya Ikhtifaa (maficho). 2- Zama ya Ghaibati ndogo. 3- Zama ya Ghaibati kubwa.

1-Zama ya Ikhtifaa (maficho)

Hii zama ya Ikhtifaa (maficho) ni wakati alipozaliwa Imam Mahdi(as) mpaka kifo cha Baba yake. Imam aliishi na Baba yake kwa muda wa miaka(5) mitano, katika muda huo Imam Askari(as) alikuwa na mamlaka makuu mawili, kwanza kumlinda Imam Mahdi(as) kutokana na maadui, na la pili kumtangaza ni Imam wa kumi na mbili wa Mashia Duniani. Watu pekee wa Nyumba ya Imam Askari(as) ndio walijua uzawa wa Imam huyo Mtukufu.

Baada ya muda Imam Askari(as) aliwakusanya Mashia  arubaini kwa ajili ya kumtambulisha Imam Mahdi(as) ni Imam wa kumi na mbili baada yake. Baada ya kuishi Samara pia alipelekwa Madina ambako huko aliishi na Babu yake kwa maficho.

2-Ghaibatu Sughra (ndogo)

Baada ya kufariki Imam Askari(as) katika mwaka wa 260 h.t  ndipo ilianza ghaibati ndogo ya Imam Mahdi(as), iliendelea ghaibati hiyo mpaka mwaka wa 329 hijiria kamaria. Katika kipindi cha ghaibati ya Imam(as) alikuwa akiwasiliana na watu maalum, ambao hao watu walikuwa wakiwasilisha masuala mbalimbali ya kidini kutoka kwa Imam mtukufu(as) watu hao ni miongoni mwa mashekhe wakubwa wa Kishia, pia kazi nyingine kubwa waliokuwa nayo ni jinsi gani ya kuwaandaa watu kwa kuipokea ghaibati kubwa ya Imam Mahdi(as)..

3-Ghaibati Kubra (kubwa)

Hiki ni kipindi kirefu cha kupotea kwa Imam Mahdi(as), kipindi hiki kilianza baada ya kuisha kupotea kipindi kifupi cha Ghaibati, kupotea kwake kurefu Imamu (as) kutaendelea kipindi hichi mpaka hapo atakapo penda Mwenyezi Mungu kumdhihirisha Imam wake.

Katika muda huu  ambao Imam hayupo, kuna Naibu wake anayeitwa kwa jina la Walii Faqih, yeye ndiye anayesimamia masuala yote ya Dini, Waislam  wote kwa ujumla wanatakiwa kumfuata na kumsikiliza katika kila jambo, mpaka hapo atakapo dhihiri Imam Mahdi Mtukufu (as).     

Imeandikwa na Dada Nuru Sudi.

maoni Viewers
Name:
Email:
* Opinion: