Hijabu
(Stara) ya kisheria ziko aina mbili: Ya dhahiri na dhati.
Ama
hijabu ya dhahiri: ni ile hijabu ambayo Mwenyezi Mungu amewaamuru wasichana na
wanawake kujihimiza kufuatilia wasifu wake, kama vile kusitiri miili yao mbele
ya wanaume ajinabi na wasio waume zao, ameamrisha hilo katika Qur’an tukufu, na
kuthibitishwa na maneno ya Mtume Mtukufu (s.a.w.w) na Maimamu masumiin (a.s).
Aidha
maulama wa fiqhi wamepambanua Zaidi suala hilo, na sisi tutaliashiria kwa muhtasari.
Wajibu
wa kuvaa hijabu ni; Msichana au mwanamke kusitiri viungo vyake kiukamilifu, ila
isipokuwa uso na mikono yake kwa wasiokuwa waume zao na ajinabi, na si maalumu
kwa juba pekee ila vazi linalositiri mwili kamili kwa wengine na kutotamanisha
maumbile yake.
Naam
yampasa atakaye kujistiri kuzingatia wa sifa
zifuatazo:
1.
Asiwe anavutia.
2.
Asiwe amevaa
mavazi yanayombana (yanachonga mwili) kiasi kwamba hudhihirisha viungo vya
mwili wake.
3.
Asivae mavazi mepesi
(yatakayoonesha viungo ambavyo ni wajibu kuvistiri).
Kama mambo hayo yalizotajwa yatakutana
katika hii stara basi itakuwa ni stara ya kisheria, hata kama katika sehemu ya mvaaji
wa stara hiyo itakuwa (vazi la) tisheti na suruali iliyo pana. Na hapa ni muhimu
kukumbusha ya kuwa pia kufunika miguu ni wajibu kwa ajinabi, na hakuna tofauti
kustiri kwa soksi au vinginevyo.
Ni
wazi kwamba; ikiwa hijabu itakuwa ni ya heshima itakuwa ni bora zaidi kuliko ya
fedheha.
Ama
hijabu ya dhati: Ni ile ambayo Mwenyezi Mungu amemuamuru Msichana na Mwanamke
kama alivyowaamuru Vijana na wanaume katika Qur’an tukufu, na
kuthibitishwa na maneno ya Mtume Muhammad (s.a.w.w) na Maimamu masumiin (a.s).
Na
madhumuni ya hijabu (stara) ya dhati ni; Ile mwanadamu kujizuia na machafu ya
ufisadi na kila kitakachomghadhibisha Mwenyezi Mungu mtukufu, kwa maana kwamba;
Uchamungu, kujiheshimu na kufumba macho kuangalia ya haramu, pia hijabu ya
dhati ni ile; Inayohusu mienendo ya Msichana na Mwanamke, aidha Mvulana na
Mwanamume, ambayo ni muhimu mno, ambapo hijabu (stara zote mbili) hukamilika
pindi iwapo nyingine, hivyo hakuna maana ya stara ila kwa kulinda taratibu
zake.
Anasema
Mwenyezi Mungu:
﴿... وَإِذَا سَأَلْتُمُوهُنَّ مَتَاعًا فَاسْأَلُوهُنَّ مِن وَرَاء
حِجَابٍ ذَلِكُمْ أَطْهَرُ لِقُلُوبِكُمْ وَقُلُوبِهِنَّ... ﴾.
"…Na
mnapo wauliza wakeze haja waulizeni nyuma ya mapazia. Hivyo ndio usafi zaidi
kwa nyoyo zenu na nyoyo zao…” Ahzaab; 53.
﴿قُل
لِّلْمُؤْمِنِينَ يَغُضُّوا مِنْ أَبْصَارِهِمْ وَيَحْفَظُوا فُرُوجَهُمْ ذَلِكَ
أَزْكَى لَهُمْ إِنَّ اللَّهَ خَبِيرٌ بِمَا يَصْنَعُونَ * وَقُل لِّلْمُؤْمِنَاتِ يَغْضُضْنَ مِنْ أَبْصَارِهِنَّ
وَيَحْفَظْنَ فُرُوجَهُنَّ وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا مَا ظَهَرَ
مِنْهَا وَلْيَضْرِبْنَ بِخُمُرِهِنَّ عَلَى جُيُوبِهِنَّ وَلَا يُبْدِينَ
زِينَتَهُنَّ إِلَّا لِبُعُولَتِهِنَّ أَوْ آبَائِهِنَّ أَوْ آبَاء بُعُولَتِهِنَّ
أَوْ أَبْنَائِهِنَّ أَوْ أَبْنَاء بُعُولَتِهِنَّ أَوْ إِخْوَانِهِنَّ أَوْ بَنِي
إِخْوَانِهِنَّ أَوْ بَنِي أَخَوَاتِهِنَّ أَوْ نِسَائِهِنَّ أَوْ مَا مَلَكَتْ
أَيْمَانُهُنَّ أَوِ التَّابِعِينَ غَيْرِ أُوْلِي الْإِرْبَةِ مِنَ الرِّجَالِ
أَوِ الطِّفْلِ الَّذِينَ لَمْ يَظْهَرُوا عَلَى عَوْرَاتِ النِّسَاء وَلَا
يَضْرِبْنَ بِأَرْجُلِهِنَّ لِيُعْلَمَ مَا يُخْفِينَ مِن زِينَتِهِنَّ وَتُوبُوا
إِلَى اللَّهِ جَمِيعًا أَيُّهَا الْمُؤْمِنُونَ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ﴾.
"Waambie
Waumini wanaume wainamishe macho yao, na wazilinde tupu zao. Hili ni takaso
bora kwao. Hakika Mwenyezi Mungu anazo khabari za wanayo yafanya. Na waambie
Waumini wanawake wainamishe macho yao, na wazilinde tupu zao, wala wasionyeshe
uzuri wao isipo kuwa unao dhihirika. Na waangushe shungi zao juu ya vifua vyao,
wala wasionyeshe uzuri wao ila kwa waume zao, au baba zao, au baba wa waume
zao, au watoto wao, au watoto wa waume zao, au kaka zao, au wana wa kaka zao,
au wana wa dada zao, au wanawake wenzao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume,
au wafuasi wanaume wasio na matamanio, au watoto ambao hawajajua mambo yaliyo
khusu uke. Wala wasipige chini miguu yao ili yajulikane mapambo waliyo yaficha. Na tubuni nyote kwa
Mwenyezi Mungu, enyi Waumini, ili mpate kufanikiwa”. An-nur, 30-31.
﴿يَا
أَيُّهَا النَّبِيُّ قُل لِّأَزْوَاجِكَ وَبَنَاتِكَ وَنِسَاء الْمُؤْمِنِينَ
يُدْنِينَ عَلَيْهِنَّ مِن جَلَابِيبِهِنَّ ذَلِكَ أَدْنَى أَن يُعْرَفْنَ فَلَا
يُؤْذَيْنَ وَكَانَ اللَّهُ غَفُورًا رَّحِيمًا﴾.
"Ewe
Nabii! Waambie wake zako, na binti zako, na wake za Waumini wajiteremshie nguo
zao. Hivyo ni karibu zaidi kuweza kutambulikana wasiudhiwe. Na Mwenyezi Mungu
ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu”. Ahzaab; 59.
و
في الختام نبتهل الى الله و نقول: اللهم ارزقنا توفيق الطاعة و بُعدَ المعصية و
صدق النية و عرفان الحرمة
.
Mwisho
tumuelekee Mwenyezi Mungu kwamuomba:
"O’
Allah! Turuzuku taufiki ya kukutii wewe na tuepushie maasi na nia njema na
maarifa ya juu ya kutambua uliyoharamisha.
و
اغضض ابصارنا عن الفجور و الخيانة
Zuia
macho yetu na maovu na hiana.
و
تفضَّل على الشباب بالانابة و التوبة
Wajaalie vijana mwelekeo bora na
toba sahihi.
و
على النساء بالحياء و العفة
.
Na
jaalia wanawake haya na uchamungu”.