bayyinaat

Published time: 07 ,February ,2017      22:48:14
“Atakaposali Mwanamke Sala zake tano, na akafunga mwezi wake mtukufu, na akalinda tupu yake, na akamtii Mumewe basi ataingia peponi kupitia mlango apendao”.
News ID: 9

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU  MWINGI WA REHEMA NA MWENYE KUREHEMU

 

Mtukufu mtume (s.a.w.w):

«إذا صلت المرأة خمسها و صامت شهرها و أحصنت فرجها و أطاعت بعلها فلتدخل من أي أبواب الجنة شاءت».

 "Atakaposali Mwanamke Sala zake tano, na akafunga mwezi wake mtukufu, na akalinda tupu yake, na akamtii Mumewe basi ataingia peponi kupitia mlango apendapo”.

Mke mwema ni hazina (yenye thamani) ya Muumini:

Imepokelewa kutoka kwa Ibn Abbas kuwa amesema: Iliposhuka Aya hii

 (...والذين يكنزون الذهب والفضة...).

"…Na ambao hukusanya dhahabu na fedha…”.

Thuban alimjia Mtume (s.a.w.w) akamuuliza: Ewe Mjumbe wa Allah; Kushuka Aya hii, ni kwa sababu ya kiburi cha Masahaba wako? Akasema (s.a.w.w): "Je! Nikueleze ni ipi hazina bora? Akasema (s.a.w.w): Ni mke mwema, ambae mumewe akimuangalia hufurahi, na akimuamuru humtii (humsikiliza), na asipokuwa naye basi humlinda”.

Utiifu wa Mke kwa mumewe sawa iwe kwa siri au dhahiri ni faradhi ambayo haihitajii mkataba za ndoa, na ikiwa Mke atakataa kumtii Mumewe basi itapekea mume kuwa mkaidi, na kuzuka mikingamo ya kifamilia, na kila atakapozidi kumtii ndipo mapenzi yatazidi baina yao, na hiyo itahamia kwa watoto wao, Hakika tabia zenye kupendana huwa ni chimbuko la kuhamia kwa watoto, wakiume kurithi kutoka kwa baba zao, na wa kike kurithi kutoka kwa Mama zao, kwani Mtume (s.a.w.w) amemhimiza sana Mwanamke kumtii mumewe, akasema: Mambo matatu hayapatwi na moto wa Jahanamu siku ya kiama: " mwanamke anayemtii Mumewe, na Mtoto mwema kwa Wazazi wake wawili, na Mja ambaye ni hakimu wa kweli kwa haki ya Mungu wake na Mkuu wake”.

Akasema tena (s.a.w.w): "Jihadi ya Mwanamke ni kuwa mke bora kwa Mumewe”. Hakika utiifu pasi na muamala mwema hautoshi, kwa Sababu Mwanamke anaweza kumtii mumewe na asiwe mwenye tabia njema kwake. Akafanya aambiwayo, na asifuatilie hatma yake, ambapo kwamba; Mwendo mzuri ni kumtii akitakacho mume, na kudhihirisha mapenzi ya kweli katika hilo, na kumuonesha mumewe tabasamu na bashasha ya kuridhika na matakwa yake, na kumsikilizisha maneno matamu, Hakika Mke kufanyia hayo basi humtuliza Mume na kumpoza roho yake.

Na yampasa Mwanamke kuzingatia nini maana ya utiifu kiukamilifu, kwani utiifu huo ndio hupelekea Mwanamke kumiliki moyo wa Mumewe, na kuchuma uaminifu wake, na kudumisha mapenzi yake, akifanya hivyo basi Mume atamkabili Mkewe kama vile Yeye ndiye anayemtii mke, na kujali apendayo Mkewe.

Hakika ni wanawake wachache ndio wanaofahamu jambo hilo, pia ni wachache ndio wanaolifanyia  kazi suala hilo, hapana shaka ya kwamba: Utiifu ndio unaokuza Shina za mapenzi baina ya wanandoa wawili, na pindi Mke atampenda mumewe kwa dhati basi hapana budi kumtimizia haki zake zote za kimsingi, yote hiyo ni picha ya matendo na alama za Mume za mapenzi zinazosababisha kutuliza moyo wake.

Minajili hiyo Mtume anasema: "Hakika Dunia ni starehe na starehe yake bora mno ni Mke mwema, utakapomuangalia (mkeo) hufurahishwa naye, na utakapomuamuru basi hukutii, na utakapomuapia hukufahamu, na ukiwa mbali naye hukulindia heshima yako na mali yako”.

Hakika huyo ni Mke mwema, mwenye upendo wa kweli, humtabasamia mumewe pindi anapomtazama kiasi kwamba mume kushindwa kuangalia mwingine zaidi yake, na wala macho ya wengine hayambabaishi maadamu yuko mwenye kumfurahisha kwa mapenzi na bashasha.

Miongoni mwa utiifu wa Mke kwa mume, ni Mke kutofunga ila kwa idhini ya mumewe, asitoke ila kwa idhini yake, asilete yeyote nyumbani kwake ila kwa idhini ya mumewe na asitumie mali yake ila kwa idhini yake, aishi pamoja na Mume kwake, na hii katika njia ya mifano iliyo wazi.

Hakika Mwanamke hawezi kutimiza haki ya Mola wake mpaka atimize ya Mumewe, na muhimu zaidi ni utiifu.  Amesema Mtukufu Mtume (s.a.w.w): "Watu watatu hazikubaliki Sala zao, wala hazipandi mbinguni amali zao njema” akata moja wapo kuwa: Mke kukasirikiwa na Mumewe hadi atakapomridhisha Mumewe.

maoni Viewers
Name:
Email:
* Opinion: