Mwanzo
Tafuta
Angalia malaika, utakuta kwamba yeye ameumbwa katika mfumo wa kwamba hana kitu kikubwa zaidi ya akili ya kutii. Mwangalie mnyama utakuta kwamba ameumbwa katika mfumo wa matamanio tu. Lakini ukirudi kwa mwanadamu utakuta kwamba kwanza amekusanya mifumo yote ambayo inapatikana kwa malaika pamoja wanyama
Kwa hakika mwenye kufunga siku moja katika mwezi wa Rajab kwa imani na matarajio basi radhi za Mwenyezi Mungu huwa ni lazima kwake, na kwa funga yake hiyo atakuwa amezima ghadhabu za Mwenyezi Mungu katika siku ile, pia hufunga mlango baina ya milango ya moto.