Mwanzo
Tafuta
Moja ya madhambi makubwa ambayo umekuja ushahidi wa wazi juu ya kuwa kwake ni ukubwa ni kula haramu kama ilivyokuja katika hadithi ya sheria ya Imam Ridhaa (a.s) katika kitabu U’yun al- akhbaar na aidha katika riwaya ya A’mash kutoka kwa Imam Sadiq (a.s), na Mwenyezi Mungu ameihesabu dhambi hii kuwa ni katika sifa za Wayahudi
Haikuishia hapo, bali ikafikia hatua ambayo Ibilisi anaweka viapo vya kuendelea kumsakama mwanadamu huyu katika maisha yake ya kila siku, ikiwa ni pamoja na kumkalia katika njia yake na kumuharibia mipango yake ya kumuelekea Mungu wake, isipokuwa waja wema ambao watakuwa wameshikamana na baadhi ya mambo ambayo kwa huyo Ibilisi yatakuwa ni kizuizi cha kuwakalia njiani.